Rais wa Sudan kusini asitisha mpango wa kutembelea Makao Makuu ya jeshi jijini Juba.

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir, amesitisha mpango wa kutembelea Makao Makuu ya jeshi jijini Juba.
Mapigano yanaendelea kushuhudiwa nchini Sudan Kusini kati ya vikosi vya serikali na waasi wa Riek Machar.
Ripoti zinasema kuwa, rais Kiir alikuwa ameanza safari ya kwenda katika makao hayo makuu Kaskazini mwa jiji kuu la Juba lakini alipofika katikati ya safari yake, aliamua kusitisha ziara yake.
Jeshi la Sudan Kusini limeendelea kushutumiwa na waangalizi wa Umoja wa Mataifa kwa kuendelea kutekeleza mashambulizi dhidi ya waasi na kusababisha maelfu ya raia w anchi hiyo kuyakimbia makwao.
Umoja wa Mataifa unasema mwaka huu pekee, watu elfu 95 wamekimbia makwao kwa sababu ya mapigano yanayoendelea.

Exit mobile version