Rais wa Sudan Kusini awafuta kazi Majaji 14

In Kimataifa

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir amewafuta kazi Majaji 14 waliokuwa wanagoma kwa muda wa miezi miwili sasa.

Kiir ametangaza hatua hiyo kupitia redio ya taifa, na kuwaambia raia wa Sudan Kusini kuwa Majaji hao wamefutwa kazi.

Inaaminiwa kuwa hatua hii imechukuliwa baada ya mgomo huo kukwamisha shughuli za Mahakama hiyo hasa jijini Juba.

Majaji hao wamekuwa wakigoma kushinikiza nyongeza ya mshahara lakini pia, kutaka kufutwa kazi kwa Jaji Mkuu Chan Reec Madut.

Madut amekuwa akishtumiwa na Majaji hao kwa kushindwa kuwatetea kuongezwa mshahara.

Mgomo huo ulimfanya rais Kiir kuunda Kamati ya kuchunguza kiini cha mgomo huo na mwezi uliopita, iliwasilisha ripoti yake kwa rais Kiir.

Hata kabla ya kufutwa kazi, Majaji hao waliamua kutorudi kazini hadi pale matakwa yao yangetekelezwa.

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu