Rais wa Sudan Kusini awafuta kazi Majaji 14

In Kimataifa

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir amewafuta kazi Majaji 14 waliokuwa wanagoma kwa muda wa miezi miwili sasa.

Kiir ametangaza hatua hiyo kupitia redio ya taifa, na kuwaambia raia wa Sudan Kusini kuwa Majaji hao wamefutwa kazi.

Inaaminiwa kuwa hatua hii imechukuliwa baada ya mgomo huo kukwamisha shughuli za Mahakama hiyo hasa jijini Juba.

Majaji hao wamekuwa wakigoma kushinikiza nyongeza ya mshahara lakini pia, kutaka kufutwa kazi kwa Jaji Mkuu Chan Reec Madut.

Madut amekuwa akishtumiwa na Majaji hao kwa kushindwa kuwatetea kuongezwa mshahara.

Mgomo huo ulimfanya rais Kiir kuunda Kamati ya kuchunguza kiini cha mgomo huo na mwezi uliopita, iliwasilisha ripoti yake kwa rais Kiir.

Hata kabla ya kufutwa kazi, Majaji hao waliamua kutorudi kazini hadi pale matakwa yao yangetekelezwa.

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu