Rais wa Sudan Kusini, Salva Kiir amesema raia wake hawajutii uamuzi wao wa kupiga kura ya kutaka uhuru wao

In Kimataifa

Rais wa Sudan Kusini, Salva Kiir amesema raia wake hawajutii uamuzi wao wa kupiga kura ya kutaka uhuru wao, licha ya kuwepo mapigano ya wenyewe kwa wenyewe katika nchi hiyo changa.

Bwana Kiir alikuwa akizungumza hayo katika maadhimisho ya miaka sita ya Uhuru kutoka Sudan.

Sherehe rasmi ziliahirishwa kutokana na vita na hali mbaya ya uchumi.

Bwana Kiir amesema imefika wakati wa kujifunza kutokana na makosa ya zamani na kuungana kuijenga Sudan Kusini.

Maelfu ya watu wamekufa, na mamilioni wamehama makazi yao, tangu mgogoro huo ulipoanza mwezi Desemba mwaka 2013.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu