Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema nchi yake haitarudi nyuma katika vita dhidi ya magaidi na wapiganaji wengine wa kijihadi nchini Mali na katika eneo la Sahel.

In Kimataifa

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema nchi yake haitarudi nyuma katika vita dhidi ya magaidi na wapiganaji wengine wa kijihadi nchini Mali na katika eneo la Sahel.

Macron ametoa kauli hii nchini Mali baada ya kuwatembelea wanajeshi wa Ufaransa katika kambi yao ya Gao Kaskazini mwa nchi hiyo.

Akiwa na rais wa nchi hiyo Ibrahim Boubacar Keita, Macron ameongeza kuwa Ujerumani pia itaendelea na nchi yake kuhakikisha kuwa magaidi hao wanashindwa.

Aidha, amesema kuwa ushirikiano wa Ufaransa na Ujerumani ni muhimu sana barani Ulaya katika maswala ya usalama lakini pia kulisaidia bara la Afrika.

Ufaransa imewatuma wanajeshi wake 1,600 Kaskazini mwa Mali kupambana na magaidi Kaskazini mwa nchi hiyo.

Hii imekuwa ni ziara ya kwanza ya rais huyu mpya barani Afrika.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu