Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema nchi yake haitarudi nyuma katika vita dhidi ya magaidi na wapiganaji wengine wa kijihadi nchini Mali na katika eneo la Sahel.

In Kimataifa

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema nchi yake haitarudi nyuma katika vita dhidi ya magaidi na wapiganaji wengine wa kijihadi nchini Mali na katika eneo la Sahel.

Macron ametoa kauli hii nchini Mali baada ya kuwatembelea wanajeshi wa Ufaransa katika kambi yao ya Gao Kaskazini mwa nchi hiyo.

Akiwa na rais wa nchi hiyo Ibrahim Boubacar Keita, Macron ameongeza kuwa Ujerumani pia itaendelea na nchi yake kuhakikisha kuwa magaidi hao wanashindwa.

Aidha, amesema kuwa ushirikiano wa Ufaransa na Ujerumani ni muhimu sana barani Ulaya katika maswala ya usalama lakini pia kulisaidia bara la Afrika.

Ufaransa imewatuma wanajeshi wake 1,600 Kaskazini mwa Mali kupambana na magaidi Kaskazini mwa nchi hiyo.

Hii imekuwa ni ziara ya kwanza ya rais huyu mpya barani Afrika.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu