Rais wa zamani wa Senegal arejea nyumbani kugombea Ubunge.

In Kimataifa
Rais wa zamani wa Senegal Abdulaye Wade amerejea nyumbani jijini Dakar kushiriki uchaguzi wa wabunge ambao umepangwa kufanyika tarehe 30 mwezi Julai mwaka huu, ambapo pia anagombea kama mbunge.
Wade mwenye umri wa miaka 91 amesema anaamini kuwa lengo lake kugombea ubunge ni kwa sababu anataka kuendelea kuwatetea raia.
Katika kampeni yake, ameshutumu serikali ya rais Macky Sall iliyoko madarakani kwa kuchochea kesi inayomkabili mtoto wake Karim Wade, ambaye anakabiliwa na kesi ya kujitajirisha kinyume cha sheria.
Wade, aliongoza Senegal kwa miaka 12 kati ya mwaka 2000 hadi mwaka 2012 na kwenda kuishi nchini Ufaransa.
Mwaka 2012, aliwania urais kwa muhula wa wa tatu lakini akashindwa baada raia wa nchi hiyo kumchagua kiongozi wa sasa Macky Sall.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu