Rais wa zamani wa Senegal arejea nyumbani kugombea Ubunge.

In Kimataifa
Rais wa zamani wa Senegal Abdulaye Wade amerejea nyumbani jijini Dakar kushiriki uchaguzi wa wabunge ambao umepangwa kufanyika tarehe 30 mwezi Julai mwaka huu, ambapo pia anagombea kama mbunge.
Wade mwenye umri wa miaka 91 amesema anaamini kuwa lengo lake kugombea ubunge ni kwa sababu anataka kuendelea kuwatetea raia.
Katika kampeni yake, ameshutumu serikali ya rais Macky Sall iliyoko madarakani kwa kuchochea kesi inayomkabili mtoto wake Karim Wade, ambaye anakabiliwa na kesi ya kujitajirisha kinyume cha sheria.
Wade, aliongoza Senegal kwa miaka 12 kati ya mwaka 2000 hadi mwaka 2012 na kwenda kuishi nchini Ufaransa.
Mwaka 2012, aliwania urais kwa muhula wa wa tatu lakini akashindwa baada raia wa nchi hiyo kumchagua kiongozi wa sasa Macky Sall.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu