Riek Machar atoa wito wa kuanza upya mazungumzo ya amani nje ya taifa linalokumbwa na vita la Sudan Kusini.

In Kimataifa
Kiongozi wa upinzani aliyeko uhamishoni Riek Machar ametoa wito wa kuanza upya mazungumzo ya amani nje ya taifa linalokumbwa na vita la Sudan Kusini.
Machar ametoa taarifa hiyo hapo jana kupitia mpatanishi wa kimataifa wa Umoja wa Mataifa, ambapo pia alikataa kukemea machafuko yanayoendelea nchini humo au kutangaza usitishwaji wa mapigano kutoka upande wake.
Hii imetokea wakati Marekani ikiwaonya viongozi nchini Sudan Kusini kuwa wako katika hatari ya kupoteza msaada wa Marekani kama watakataa kushiriki katika mazungumzo ya amani na kuheshimu muda uliowekwa wa kusitishwa mapigano.
 Maelfu ya watu wameuawa na zaidi ya milioni 3.5 wamekimbia makazi yao baada ya Rais Salva Kiir kumtuhumu aliyekuwa naibu wake Machar kwa kupanga njama ya mapinduzi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu