Ronaldo amkalisha Messi kwenye Ballon d’Or, Akaribia kukalia kiti chake.

In Kimataifa, Michezo

Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Ureno na klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo ametwaa tuzo ya Ballon d’Or kwa mwaka wa pili mfululizo usiku wa kuamkia leo.

Ronaldo amemshinda mpinzani wake wa karibu anayekipiga kunako klabu ya Barcelona, Lionel Messi, katika tuzo hiyo na kuweza kutwaa kwa mara ya tano.

Kwa ushindi huo sasa Ronaldo na Messi wote wanakuwa sawa kwa kuchukua tuzo hiyo kubwa ya heshima mara tano.

Nyota wa Barcelona Lionel Messi, amepata nafasi ya pili huku mshambuliaji wa PSG, Neymar Jr akishika nafasi ya tatu. Kama kura zinavyoonesha (1. Cristiano Ronaldo -946 pts 2. Lionel Messi -670 pts 3. Neymar -370 pts)

Lionel Messi ndiye mchezaji pekee aliyekuwa mwenye mataji mengi ya tuzo hiyo kabla ya jana Ronaldo kuchukua tuzo hiyo na kumfanya awe naye sawa kitu ambacho endapo Messi atazubaa msimu huu basi ufalme huo wa kumiliki kwa wingi tuzo hiyo huenda akachukua Ronaldo.

Msimu uliopita Ronaldo aliisaidia timu yake ya Real Madrid kutwaa ubingwa wa klabu bingwa barani Ulaya na ubingwa wa la Liga kwa mara ya kwanza toka toka mwaka 2012.

Ballon d’Or ni tuzo ambayo imekua ikitolewa na jarida la nchini Ufaransa toka mwaka 1956 na kura hupigwa na waandishi wa habari wapatao 173, duniani kote.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu