Ronaldo amkalisha Messi kwenye Ballon d’Or, Akaribia kukalia kiti chake.

In Kimataifa, Michezo

Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Ureno na klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo ametwaa tuzo ya Ballon d’Or kwa mwaka wa pili mfululizo usiku wa kuamkia leo.

Ronaldo amemshinda mpinzani wake wa karibu anayekipiga kunako klabu ya Barcelona, Lionel Messi, katika tuzo hiyo na kuweza kutwaa kwa mara ya tano.

Kwa ushindi huo sasa Ronaldo na Messi wote wanakuwa sawa kwa kuchukua tuzo hiyo kubwa ya heshima mara tano.

Nyota wa Barcelona Lionel Messi, amepata nafasi ya pili huku mshambuliaji wa PSG, Neymar Jr akishika nafasi ya tatu. Kama kura zinavyoonesha (1. Cristiano Ronaldo -946 pts 2. Lionel Messi -670 pts 3. Neymar -370 pts)

Lionel Messi ndiye mchezaji pekee aliyekuwa mwenye mataji mengi ya tuzo hiyo kabla ya jana Ronaldo kuchukua tuzo hiyo na kumfanya awe naye sawa kitu ambacho endapo Messi atazubaa msimu huu basi ufalme huo wa kumiliki kwa wingi tuzo hiyo huenda akachukua Ronaldo.

Msimu uliopita Ronaldo aliisaidia timu yake ya Real Madrid kutwaa ubingwa wa klabu bingwa barani Ulaya na ubingwa wa la Liga kwa mara ya kwanza toka toka mwaka 2012.

Ballon d’Or ni tuzo ambayo imekua ikitolewa na jarida la nchini Ufaransa toka mwaka 1956 na kura hupigwa na waandishi wa habari wapatao 173, duniani kote.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu