Ronaldo anyakua tuzo kwa mara nyingine tena.

In Kimataifa, Michezo

Kwa mara ya pili Cristiano Ronaldo ametwaa tuzo ya The Best Fifa awards baada ya kupata 43% ya kura zilizopigwa huku akimuacha mbali mpinzani wake mkubwa Lioneil Messi aliyepata 19%.


Msimu uliopita Cristiano Ronaldo alifunga mabao 12 katika Champions League huku akifunga mara mbili katika mchezo wa fainali na kuwasaidia Real Madrid kutetea kombe la Champions League.


Manahodha waliompigia kura Cristiano Ronaldo ni pamoja na Luca Modric, Sergio Ramos, na Marcelo huku Neymar, Iniesta na Suarez wakimpigia kura Lioneil Messi.

Wakati Ronaldo akitwaa Best Male awards kocha wake Zinedine Zidane aliwabwaga Massimiliano Allegri na Antonio Conte na kutwaa tuzo ya kocha bora wa FIFA.


Gianluigi Buffon alichukua tuzo ya golikipa bora akiwabwaga wapinzani wake golikipa wa Real Madrid Keylor Navas na golikipa wa Bayern Munich Manuel Neuer.


Olivier Giroud alipata tuzo ya bao bora huku kikosi bora cha Fifa kikiundwa na Gianluigi Bufgon, Dani Alves,Leornardo Bonuccci, Sergio Ramos, Marcelo,Toni Kroos, Andres Iniesta, Luvca Modric, Cristiano Ronaldo, Lioneil Messi na Neymar.

Tuzo zingine zilizotolewa usiku wa leo ni tuzo ya mchezaji bora wa kike iliyokwenda kwa Lieke Mertenes, tuzo ya kocha bora wa kike ikienda kwa Sarina Wiegman na tuzo ya mashabiki ikienda kwa mashabiki wa Celtic.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

ZOEZI LA UOKOAJI HANANG, MAWAZIRI WAFIKA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama, Waziri wa Ujenzi Innocent

Read More...

RC MBEYA AFANYA UZINDUZI ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO VYA (NIDA)

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mhe. Comrede Juma Zuberi Homera amefanya uzinduzi wa wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho

Read More...

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu