RPC Geita kathibitisha kukamatwa kwa Mh. Musukuma.

In Kitaifa

 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita Mponjoli Mwabulambo amethibitisha kuwa Jeshi la Polisi linamshikilia Mbunge na Mwenyekiti wa CCM Geita, Joseph Musukuma baada ya kukamatwa September 17, 2017 na baadhi ya Madiwani wa Mkoa huo.

Kamanda Mponjoli Mwabulambo amesema bado Mbunge Musukuma na wenzie na wanafanyiwa mahojiano juu ya kilichotokea huku akisema idadi ya watu wenye makosa ikiongezeka.

Na kwa upande mwingine Kamanda Mponjoli amesema Mh.Musukuma alikamatwa na Polisi na sio kuwa aliripoti Kituoni kwa hiari yake kama habari zilivyosambaaya kuwa Mh.Musukuma aliripoti kwa hiari yake.

Lakini pia Kamnda Mponjoli amethibitisha ya kuwa Mh.Musukuma amepelekwa Mahakamani asubuhi ya leo

Kama ulikua ufahamu kuhusiana na ishu hii ya kukamatwa na kupelekwa Mahakamani kwa Mbunge Musukuma ni kwamba;

Mbunge Musukuma pamoja na baadhi ya wadiwani na wananchi, walikamatwa na polisi kwa kufunga njia inayoeleka kwenye mgodi wa GGM na kuleta vurugu, kushinikiza mgodi huo kulipa dola milioni 12.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu