RUTO IMF KUONGEZA MSAMAHA WA MADENI

In Kimataifa

Rais William Ruto ametoa wito kwa mashirika ya fedha duniani kupanua msamaha wa deni la umma kwa nchi zinazoendelea katika hotuba yake ya kwanza kama mkuu wa nchi katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York.

Akitoa hotuba yake mbele ya viongozi mbalimbali kote duniani, Kiongozi huyo alibainisha kuwa nchi nyingi bado zinaendelea kupata afueni kutokana na athari mbaya za janga la Covid-19 na msamaha wa madeni utasaidia sana kufanikisha miradi ya maendeleo ambayo tayari imeanzishwa na nchi hizo.

Ruto, ambaye amekuwa ofisini kwa muda wa wiki moja, alisema kuwa Kenya, kama nchi nyingine za kipato cha kati, bado inakabiliana na kushuka kwa uchumi na shinikizo la mfumuko wa bei hivyo basi haja ya kurekebisha mipango ya ulipaji wa mkopo.

“Kwa niaba ya Kenya, ninaungana na viongozi wengine kutoa wito kwa Benki ya Dunia, Shirika la Fedha la Kimataifa na wakopeshaji wengine wa kimataifa kupanua misamaha ya madeni yanayohusiana na janga kwa nchi zilizoathiriwa zaidi, haswa zile zilizoathiriwa na mchanganyiko mbaya wa migogoro , mabadiliko ya hali ya hewa na Covid-19,” Dkt Ruto alinukuliwa na gzeti la Nation Daily akisema.

.

Kulingana na Daily Nation, Ruto Pia ametoa wito kwa nchi nyingine kushirikiana na nchi zinazoendelea kusaidia katika kukabiliana na janga hili.

“Kenya na Afrika nzima, kama nchi nyingine zinazoendelea, zinahitaji ushirikiano wa kimataifa ili kuepusha mzozo wa kiuchumi kutokana na janga hili,” alinukuliwa na gazeti la Nation akiongezea.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu