SACP Fortunatus Musilimu amefanya ziara ya kushtukiza Kituo Kikuu cha Mabasi.

In Kitaifa

Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, SACP Fortunatus Musilimu amefanya ziara ya kushtukiza Kituo Kikuu cha Mabasi yaendayo Mikoani na Nchi jirani, Ubungo na kuzindua uwekaji wa namba za simu kwenye mabasi kwa ajili ya abiria kutoa taarifa pale madereva wanapokiuka sheria za Usalama barabarani.

Kamanda Musilimu ameeleza kuwa hatua hiyo ni kusaidia abiria kutoa taarifa pindi madereva wanapokiuka sheria za Usalama Barabarani na kuhatarisha maisha yao, na kusema zoezi hilo ni la nchi nzima ambalo litakuwa endelevu na ukaguzi wa mara kwa mara utafanyika kuhakikisha namba hizo hazitolewi kwenye mabasi hayo.

Lakini pia Kamanda Musilimu ametoa onyo kali kwa madereva na makondakta watakao ziondoa namba hizo katika mabasi, kwani kufanya hivyo ni kosa kisheria na kuwaasa kuziacha namba hizo katika mabasi yao ili wasafiri waweze kuzitumia.

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu