SACP Fortunatus Musilimu amefanya ziara ya kushtukiza Kituo Kikuu cha Mabasi.

In Kitaifa

Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, SACP Fortunatus Musilimu amefanya ziara ya kushtukiza Kituo Kikuu cha Mabasi yaendayo Mikoani na Nchi jirani, Ubungo na kuzindua uwekaji wa namba za simu kwenye mabasi kwa ajili ya abiria kutoa taarifa pale madereva wanapokiuka sheria za Usalama barabarani.

Kamanda Musilimu ameeleza kuwa hatua hiyo ni kusaidia abiria kutoa taarifa pindi madereva wanapokiuka sheria za Usalama Barabarani na kuhatarisha maisha yao, na kusema zoezi hilo ni la nchi nzima ambalo litakuwa endelevu na ukaguzi wa mara kwa mara utafanyika kuhakikisha namba hizo hazitolewi kwenye mabasi hayo.

Lakini pia Kamanda Musilimu ametoa onyo kali kwa madereva na makondakta watakao ziondoa namba hizo katika mabasi, kwani kufanya hivyo ni kosa kisheria na kuwaasa kuziacha namba hizo katika mabasi yao ili wasafiri waweze kuzitumia.

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu