Saudi Arabia kusitisha kununua silaha kutoka Ujerumani na kansela Angel Merkel atoa wito Ghuba kuacha mashambulizi ya anga nchini Yemen.

In Kimataifa

Saudi Arabia inasema haitaki tena kununua silaha kutoka Ujerumani, kauli inayokuja wakati Kansela Angela Merkel akitoa wito kwa taifa hilo kubwa la Ghuba kuacha mashambulizi ya anga nchini Yemen.

Kansela Merkel aliwasili jana nchini Saudi Arabia kwa ziara ya kikazi. Naibu Waziri wa Uchumi wa Saudia, Mohammed al-Tuwaijiri, ameliambia jarida la “Der Spiegel” la hapa Ujerumani kwamba sasa nchi yake itajizuwia kuomba silaha zaidi kutoka Ujerumani, na badala yake kujielekeza kwenye ushirikiano wa kiuchumi na sekta nyengine.

Al-Tuwaijiri amesema kuwa Saudia inayafahamu mazingira ya kisiasa yalivyo na haitaki kusababisha matatizo zaidi kwa serikali ya Ujerumani, akisisitiza kuwa Ujerumani na Saudia zina mambo mengine muhimu zaidi kuliko silaha.

Akiwa na ujumbe mkubwa wa wafanyabiashara, Kansela Merkel alipokewa na kufanya mazungumzo na Mfalme Salman na warithi wake hapo jana, ikiwa ziara yake ya kwanza baada ya miaka saba nchini Saudia.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu