Saudi Arabia kusitisha kununua silaha kutoka Ujerumani na kansela Angel Merkel atoa wito Ghuba kuacha mashambulizi ya anga nchini Yemen.

In Kimataifa

Saudi Arabia inasema haitaki tena kununua silaha kutoka Ujerumani, kauli inayokuja wakati Kansela Angela Merkel akitoa wito kwa taifa hilo kubwa la Ghuba kuacha mashambulizi ya anga nchini Yemen.

Kansela Merkel aliwasili jana nchini Saudi Arabia kwa ziara ya kikazi. Naibu Waziri wa Uchumi wa Saudia, Mohammed al-Tuwaijiri, ameliambia jarida la “Der Spiegel” la hapa Ujerumani kwamba sasa nchi yake itajizuwia kuomba silaha zaidi kutoka Ujerumani, na badala yake kujielekeza kwenye ushirikiano wa kiuchumi na sekta nyengine.

Al-Tuwaijiri amesema kuwa Saudia inayafahamu mazingira ya kisiasa yalivyo na haitaki kusababisha matatizo zaidi kwa serikali ya Ujerumani, akisisitiza kuwa Ujerumani na Saudia zina mambo mengine muhimu zaidi kuliko silaha.

Akiwa na ujumbe mkubwa wa wafanyabiashara, Kansela Merkel alipokewa na kufanya mazungumzo na Mfalme Salman na warithi wake hapo jana, ikiwa ziara yake ya kwanza baada ya miaka saba nchini Saudia.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Trump apiga marufuku raia wa mataifa 12 kuingia Marekani

Rais wa Marekani Donald Trump ametia saini tangazo jipya linaloweka marufuku kali kwa raia wa mataifa 12 kuingia nchini

Read More...

Serikali Yafuta Usajili wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Linaloongozwa na Askofu Gwajima

Serikali kupitia Msajili wa Jumuiya za Kiraia, Emmanuel Kihampa, imetangaza kulifutia usajili Kanisa la Ufufuo na Uzima linaloongozwa na

Read More...

KATIBA YA CCM YAFANYIWA MABADILIKO 

Kwa mujibu wa taarifa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu