Saudi Arabia kusitisha kununua silaha kutoka Ujerumani na kansela Angel Merkel atoa wito Ghuba kuacha mashambulizi ya anga nchini Yemen.

In Kimataifa

Saudi Arabia inasema haitaki tena kununua silaha kutoka Ujerumani, kauli inayokuja wakati Kansela Angela Merkel akitoa wito kwa taifa hilo kubwa la Ghuba kuacha mashambulizi ya anga nchini Yemen.

Kansela Merkel aliwasili jana nchini Saudi Arabia kwa ziara ya kikazi. Naibu Waziri wa Uchumi wa Saudia, Mohammed al-Tuwaijiri, ameliambia jarida la “Der Spiegel” la hapa Ujerumani kwamba sasa nchi yake itajizuwia kuomba silaha zaidi kutoka Ujerumani, na badala yake kujielekeza kwenye ushirikiano wa kiuchumi na sekta nyengine.

Al-Tuwaijiri amesema kuwa Saudia inayafahamu mazingira ya kisiasa yalivyo na haitaki kusababisha matatizo zaidi kwa serikali ya Ujerumani, akisisitiza kuwa Ujerumani na Saudia zina mambo mengine muhimu zaidi kuliko silaha.

Akiwa na ujumbe mkubwa wa wafanyabiashara, Kansela Merkel alipokewa na kufanya mazungumzo na Mfalme Salman na warithi wake hapo jana, ikiwa ziara yake ya kwanza baada ya miaka saba nchini Saudia.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu