Saudi Arabia kusitisha kununua silaha kutoka Ujerumani na kansela Angel Merkel atoa wito Ghuba kuacha mashambulizi ya anga nchini Yemen.

In Kimataifa

Saudi Arabia inasema haitaki tena kununua silaha kutoka Ujerumani, kauli inayokuja wakati Kansela Angela Merkel akitoa wito kwa taifa hilo kubwa la Ghuba kuacha mashambulizi ya anga nchini Yemen.

Kansela Merkel aliwasili jana nchini Saudi Arabia kwa ziara ya kikazi. Naibu Waziri wa Uchumi wa Saudia, Mohammed al-Tuwaijiri, ameliambia jarida la “Der Spiegel” la hapa Ujerumani kwamba sasa nchi yake itajizuwia kuomba silaha zaidi kutoka Ujerumani, na badala yake kujielekeza kwenye ushirikiano wa kiuchumi na sekta nyengine.

Al-Tuwaijiri amesema kuwa Saudia inayafahamu mazingira ya kisiasa yalivyo na haitaki kusababisha matatizo zaidi kwa serikali ya Ujerumani, akisisitiza kuwa Ujerumani na Saudia zina mambo mengine muhimu zaidi kuliko silaha.

Akiwa na ujumbe mkubwa wa wafanyabiashara, Kansela Merkel alipokewa na kufanya mazungumzo na Mfalme Salman na warithi wake hapo jana, ikiwa ziara yake ya kwanza baada ya miaka saba nchini Saudia.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu