Sekta ya utalii nchini Kenya imepigwa jeki baada ya rais Uhuru Kenyatta kufungua hoteli mbili mbali na kuzindua ujenzi wa jumba refu barani Afrika.

In Kimataifa

Sekta ya utalii nchini Kenya imepigwa jeki baada ya rais Uhuru Kenyatta kufungua hoteli mbili mbali na kuzindua ujenzi wa jumba refu barani Afrika.

Hoteli hizo mbili zitakazojulikana kwa jina Nairobi Hotels, ni hoteli ya Park Inn iliopo eneo la Westlands iliyo na vitanda 140 na kusimamiwa na Radisson Hotel na Lazizi Premier ilio na vitanda 144 na itakuwa hoteli ya kwanza ya kifahari itakayokuwa karibu na uwanja wa ndege.

Rais pia aliweka jiwe la msingi la Jumba la Pinnacle Tower ambalo litakuwa refu zaidi barani Afrika.

Jengo hilo litakalojengwa katika eneo la Upper Hill jijini nairobi, litakuwa na ghorofa 70 na urefu wa futi 900 hivyobasi kulifanya kuwa refu zaidi barani.

Jumba hilo litakuwa na ofisi za kibiashara nyumba za kukodisha na Hoteli ya Hilton Hotel mbali na kuwa na duka la jumla na kituo cha burudani.

Kwa sasa jumbe refu zaidi barani Afrika ni lile la Carlton Center lililopo mjini Johannesburg nchini Afrika Kusini.

Limekuwa jumba refu zaidi kwa kipindi cha miaka 39 hadi kufikia sasa.

Jumba la Pinnacle Towers litakuwa miongoni mwa majumba marefu duniani.

Jumba la Dubai Burj Khalifa ndio refu zaidi duniani likiwa na urefu wa mita 800.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu