SERENGETI BOYS WATUA SALAMA MOROCCO

Baada ya safari ndefu, hatimaye kikosi cha Serengeti Boys kimetua salama nchini Morocco.

Serengeti imetua Morocco tayari kuweka kambi kujiandaa na michuano ya Kombe la Mataifa Afrika nchini Gabon.

Mwenyekiti wa Soka la Vijana wa TFF, Ayubu Nyenzi amesema wamefika salama Casablanca lakini wanalazimika kusafiri kilomita 100 zaidi.

“Tunatoka Casablanca kwenda Rabat, hivyo safari inaendelea safari hii kwa gari,” alisema.

Kikosi hicho kiliondoka jana Alasiri kwenda Morocco kupitia Dubai, safari ambayo imechukua zaidi ya saa 24 kukamilika.

Exit mobile version