Serikali imerejea kauli yake ya kuhakikisha watu wanaofanya mauaji ya polisi na viongozi wa Chama cha Mapinduzi katika wilaya za Kibiti na Rufiji Mkoani Pwani wanakamatwa na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

In Kitaifa

Serikali imerejea kauli yake ya kuhakikisha watu wanaofanya mauaji ya polisi na viongozi wa Chama cha Mapinduzi katika wilaya za Kibiti na Rufiji Mkoani Pwani wanakamatwa na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi Mwigulu Nchemba amesisitiza kuwa operesheni maalum inayoendelea katika wilaya hizo ni lazima itoe matokeo yatakayomhakikishia kila mwananchi maisha salama ndani ya nchi hii.

Ametoa kauli hiyo wakati alipofanya ziara ya kukagua kambi maalum ya operesheni ya kuwatafuta wauaji wa baadhi ya viongozi wa chama cha mapinduzi wilayani Kibiti, akiwa ameambatana na Mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoani Pwani ambaye pia ni mkuu wa Mkoa huo Mhandisi Evarist Ndikilo.

Katika maelezo yake, Waziri huyo wa mambo ya ndani amesema hisia zilizokuwepo kwamba pengine mauaji hayo yanahusishwa na katazo la biashara ya mazao ya misitu ukiwemo mkaa, misimamo ya kidini, Ujambazi ama ugaidi siyo za kweli, bali ni mchezo uliobuniwa na kundi la watu kwa sababu ambazo haziko wazi na kwa hiyo ni lazima vitendo hivyo vikomeshwe mara moja.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu