Serikali imerejea kauli yake ya kuhakikisha watu wanaofanya mauaji ya polisi na viongozi wa Chama cha Mapinduzi katika wilaya za Kibiti na Rufiji Mkoani Pwani wanakamatwa na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

In Kitaifa

Serikali imerejea kauli yake ya kuhakikisha watu wanaofanya mauaji ya polisi na viongozi wa Chama cha Mapinduzi katika wilaya za Kibiti na Rufiji Mkoani Pwani wanakamatwa na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi Mwigulu Nchemba amesisitiza kuwa operesheni maalum inayoendelea katika wilaya hizo ni lazima itoe matokeo yatakayomhakikishia kila mwananchi maisha salama ndani ya nchi hii.

Ametoa kauli hiyo wakati alipofanya ziara ya kukagua kambi maalum ya operesheni ya kuwatafuta wauaji wa baadhi ya viongozi wa chama cha mapinduzi wilayani Kibiti, akiwa ameambatana na Mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoani Pwani ambaye pia ni mkuu wa Mkoa huo Mhandisi Evarist Ndikilo.

Katika maelezo yake, Waziri huyo wa mambo ya ndani amesema hisia zilizokuwepo kwamba pengine mauaji hayo yanahusishwa na katazo la biashara ya mazao ya misitu ukiwemo mkaa, misimamo ya kidini, Ujambazi ama ugaidi siyo za kweli, bali ni mchezo uliobuniwa na kundi la watu kwa sababu ambazo haziko wazi na kwa hiyo ni lazima vitendo hivyo vikomeshwe mara moja.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu