Serikali imesisitiza kuwa sera ya Afya ya mwaka 2007 inaeleza kuwa huduma za kina mama wajawazito katika vituo vya ngazi zote zinatakiwa kutolewa bila malipo.

In Kitaifa

Serikali imesisitiza kuwa sera ya Afya ya mwaka 2007 inaeleza kuwa huduma za kina mama wajawazito katika vituo vya ngazi zote zinatakiwa kutolewa bila malipo.

Kauli hiyo imetolewa leo Bungeni Mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Dk.Khamis Kigwangala,wakati akijibu swali la mbunge wa Viti Maalum, Manira Musta  Khatibu,aliyetaka kujua  Serikali ina mpango gani wa kufuta tozo na gharama za vifaa vya kujifungulia na upasuaji kama ilivyofuta za matibabu ya wazee na wagonjwa wa kisukari.

Dk.Kigwangala amesema serikali haijawai kuweka tozo na gharama za vifaa vya kujifungulia na upasuaji.Amesema huduma hizo zinatolewa katika ngazi zote katika vituo vya Umma vya kutolea huduma kwa gharama za serikali.

Hata hivyo amesema ili kuhakikisha sera hiyo inatekelezwa kwa vitendo,wizara inahakikisha akina mama wanakuwa na vifaa muhimu vya kujifungulia, ambapo vifuko maalum vyenye vifaa vya kujifungulia kwa wanawake 500,000 vitasamazwa nchi nzima kulingana na uhitaji.

Katika hatua nyingine Dk.Kigwangala amesema kuwa kutokana na sera ya afya kwa sasa serikali imejikita zaidi katika kuimalisha sekta ya afya.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu