Serikali imesisitiza kuwa sera ya Afya ya mwaka 2007 inaeleza kuwa huduma za kina mama wajawazito katika vituo vya ngazi zote zinatakiwa kutolewa bila malipo.

In Kitaifa

Serikali imesisitiza kuwa sera ya Afya ya mwaka 2007 inaeleza kuwa huduma za kina mama wajawazito katika vituo vya ngazi zote zinatakiwa kutolewa bila malipo.

Kauli hiyo imetolewa leo Bungeni Mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Dk.Khamis Kigwangala,wakati akijibu swali la mbunge wa Viti Maalum, Manira Musta  Khatibu,aliyetaka kujua  Serikali ina mpango gani wa kufuta tozo na gharama za vifaa vya kujifungulia na upasuaji kama ilivyofuta za matibabu ya wazee na wagonjwa wa kisukari.

Dk.Kigwangala amesema serikali haijawai kuweka tozo na gharama za vifaa vya kujifungulia na upasuaji.Amesema huduma hizo zinatolewa katika ngazi zote katika vituo vya Umma vya kutolea huduma kwa gharama za serikali.

Hata hivyo amesema ili kuhakikisha sera hiyo inatekelezwa kwa vitendo,wizara inahakikisha akina mama wanakuwa na vifaa muhimu vya kujifungulia, ambapo vifuko maalum vyenye vifaa vya kujifungulia kwa wanawake 500,000 vitasamazwa nchi nzima kulingana na uhitaji.

Katika hatua nyingine Dk.Kigwangala amesema kuwa kutokana na sera ya afya kwa sasa serikali imejikita zaidi katika kuimalisha sekta ya afya.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu