Serikali inaifanyia marekebisho Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), kwa kuongeza watalaamu waliobobea katika fani hiyo ili kuandaa vitabu bora.

In Kitaifa

Serikali inaifanyia marekebisho Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), kwa kuongeza watalaamu waliobobea katika fani hiyo ili kuandaa vitabu bora.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ametoa mkakati huo wa Serikali bungeni jana wakati akijibu swali la Mbunge wa Vunjo, James Mbatia (NCCR-Mageuzi).

Mbatia alimuuliza swali la papo hapo Waziri Mkuu, la nini mkakati wa Serikali katika kuondoa vitabu ambavyo vilionekana kwamba vina makosa.

Waziri Mkuu amesema serikali inashughulikia jambo hilo kwa kuiboresha TEA ambapo tayari Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi analifanyia kazi hilo tangu wakati Mkurugenzi Mkuu wa Tea amewajibishwa kutokana na vitabu vibovu.

Amesema Serikali imekusudia kuiboresha kwa kutumia wasomi waliobobea katika fani hiyo kutoka vyuo vikuu nchini na katika taasisi nyingine kwenda kwenye taasisi hiyo kuandaa vitabu bora.

Waziri Mkuu alikiri kwamba hapo awali kulitokea tatizo kidogo wa uchapishaji vitabu bora wakati serikali ilipoachia kazi hiyo mtu mmoja mmoja kuandaa vitabu vya kiada na ziada.

Waziri Mkuu amesema sera ni kitu kingine, vitabu vinaandaliwa kutokana na sera, mtaala, silabasi na inapendeleza somo lipi liandaliwe katika vitabu gani vya msingi na vya kiada na ziada.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu