Serikali ipo tayari kumtibu Tundu Lissu.

In Afya, Kitaifa

Dar es Salaam. Serikali imesema ipo tayari kugharamia matibabu zaidi ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu popote duniani.

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu ameeleza hayo leo Alhamis kuwa watafanya hivyo pindi watakapopata maombi kutoka kwa familia pamoja na taarifa kutoka kwa madaktari kuhusu mahitaji ya matibabu zaidi ya mgonjwa.

Taarifa hiyo ya Ummy imekuja muda mfupi baada ya Mbunge wa  Singida Kaskazini(CCM), Lazaro  Nyalandu akusema kwamba madaktari wa Kenya wamesema Lissu  hawezi kusafirishwa kwenda nje kwa ajili ya kumpatiwa matibabu.

Mbunge Nyalandu ameeleza hayo kwenye ukurasa wake wa Instagram, Facebook na Twitter  kwamba  mipango ya kumsafirisha  Lissu ambayo walikuwa wanafanya itasimama kwa sasa  kutokana na ushauri wa madaktari hao  ili kuruhusu kukamilishiwa huduma za tiba ambazo tayari ameanzishiwa, hadi hapo itakavyoshauriwa vinginevyo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu