Serikali ipo tayari kumtibu Tundu Lissu.

In Afya, Kitaifa

Dar es Salaam. Serikali imesema ipo tayari kugharamia matibabu zaidi ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu popote duniani.

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu ameeleza hayo leo Alhamis kuwa watafanya hivyo pindi watakapopata maombi kutoka kwa familia pamoja na taarifa kutoka kwa madaktari kuhusu mahitaji ya matibabu zaidi ya mgonjwa.

Taarifa hiyo ya Ummy imekuja muda mfupi baada ya Mbunge wa  Singida Kaskazini(CCM), Lazaro  Nyalandu akusema kwamba madaktari wa Kenya wamesema Lissu  hawezi kusafirishwa kwenda nje kwa ajili ya kumpatiwa matibabu.

Mbunge Nyalandu ameeleza hayo kwenye ukurasa wake wa Instagram, Facebook na Twitter  kwamba  mipango ya kumsafirisha  Lissu ambayo walikuwa wanafanya itasimama kwa sasa  kutokana na ushauri wa madaktari hao  ili kuruhusu kukamilishiwa huduma za tiba ambazo tayari ameanzishiwa, hadi hapo itakavyoshauriwa vinginevyo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu