Serikali katika mwaka wa fedha 2017/18, imetenga Sh bilioni 56 kwa ajili ya kufanya ukarabati majengo na mabweni katika vyuo vikuu mbalimbali nchini.

In Kitaifa

Serikali katika mwaka wa fedha 2017/18, imetenga Sh bilioni 56 kwa ajili ya kufanya ukarabati majengo na mabweni katika vyuo vikuu mbalimbali nchini.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Stella Manyanya alisema ukarabati huo utahusisha pia majengo ya Chuo Kikuu Mzumbe, Morogoro. Manyanya alisema ameshatoa ushauri kwa viongozi wa chuo hicho kuhakikisha wanatumia fedha za ndani kuhakikisha wanafanya ukarabati wa miundombinu ya maji katika chuo hicho.

Amesema pia ukarabati huo utaenda sambamba na ujenzi wa bweni la Chuo Kikuu Huria (OUT) Dodoma, ukarabati wa majengo ya Chuo Kikuu cha Ushirika na Biashara Moshi (MUCCOBS), ujenzi wa mabweni uliofanyika Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM) na Chuo Kishiriki cha Elimu (Duce).

Akijibu swali la msingi la Mbunge wa Viti Maalumu, Asha Juma (CCM) aliyetaka kujua kuna utaratibu gani wa kuyafanyia ukarabati majengo ya Chuo Kikuu Mzumbe Morogoro, Manyanya alisema serikali imeanza ukarabati wa miundombinu na majengo katika kampasi ya Chuo Kikuu cha Mzumbe, Morogoro kwa gharama ya Sh bilioni mbili.

Amesema hadi kufikia Mei 31 mwaka huu, Sh milioni 884.6 zilizotengwa zilikwishatolewa na wizara na inaendelea kufuatilia hizo zilizobaki ili zitolewe kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha.

Amesema kwa juhudi hizo za ukarabati unaoendelea kutekelezwa chuoni hapo ni dhahiri serikali ina nia ya dhati ya kuinua hadhi ya chuo hicho, kuweka mazingira stahiki ya kufundishia na kujifunzia pamoja na kuwapunguzia adha wasichana .

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu