Serikali kutangaza haraka nafasi za ajira katika sekta ya afya.

In Kitaifa
SERIKALI inakusudia kutangaza haraka nafasi za ajira katika sekta ya afya baada ya  baadhi ya wafanyakazi wake kuacha kazi kutokana na kuwa na vyeti feki na kusababisha zahanati na vituo  vya  afya  kuanza kufungwa kwa kukosa watumishi.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amebainisha hayo  leo kwenye maadhimisho ya siku ya waaguzi duniania yalioyofanyika  Kitaifa katika mji wa Itigi Wilaya ya Manyoni Mkoani Singida.
Waziri Mwalimu amesema kuwa suala la vyeti feki limewakumba zaidi wauguzi na  tayari  Rais John Magufuli ametoa kibali cha kuajiri wengine ili kuwazesha wananchi kuendelea kupata huduma katika sekta ya afya.
Amefafanua kuwa  suala hilo litakwenda sanjari na  ajira nyingine  za kawaida ili kupunguza uhaba  wa watumishi katika sekta hiyo.
 Awali katika taarifa  zao  Katibu wa Chama Cha  Wauguzi  Nchini Sebastian Luziga na Rais wake Paul Magesa wametaka kutatuliwa kwa changamoto za ukosefu wa dawa, vifaa tiba na maslahi kwa watumishi.
Hivi  Karibuni Rais Dr John Magufuli alitangaza kuwafukuza kazi watumishi wa   umma zaidi ya 9,000 kutokana na kuwa na vyeti feki

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu