Serikali Mkoani Kilimanjaro imeliagiza Jeshi la Polisi Mkoani hapo, kufanya ukaguzi maalumu wa magari yanayobeba wanafunzi hususani shule binafsi

In Kitaifa

Serikali Mkoani Kilimanjaro imeliagiza    Jeshi la Polisi Mkoani hapo, kufanya ukaguzi maalumu wa magari yanayobeba wanafunzi hususani shule binafsi ,ili kujiridhisha kama yana sifa ya kufanya kazi hiyo.

Mkuu wa mkoa huo, Saidi Mecki Sadiki amesema hayo wakati wa Kikao cha Ushauri cha Mkoa (RCC) ,ambacho kilikuwa maalumu kwa suala la hifadhi ya mazingiraambapo amekitaka  Kikosi cha usalama barabarani kiandae mpango wa ukaguzi wa magari ya wanafunzi kila Jumamosi, na yale yasiyo na sifa yaondolewe barabarani.

Sadiki amesema Serikali ilisikitishwa na vifo vya watu wasio na hatia ,kwani pia katika ajali hiyo mkoa wake uliguswa kwa kupoteza watoto 14.

Aidha amemtaka Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Hamisi Issa kusimamia kikamilifu ukaguzi huo ili kuepuka udanganyifu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu