Serikali Mkoani Kilimanjaro imeliagiza Jeshi la Polisi Mkoani hapo, kufanya ukaguzi maalumu wa magari yanayobeba wanafunzi hususani shule binafsi

In Kitaifa

Serikali Mkoani Kilimanjaro imeliagiza    Jeshi la Polisi Mkoani hapo, kufanya ukaguzi maalumu wa magari yanayobeba wanafunzi hususani shule binafsi ,ili kujiridhisha kama yana sifa ya kufanya kazi hiyo.

Mkuu wa mkoa huo, Saidi Mecki Sadiki amesema hayo wakati wa Kikao cha Ushauri cha Mkoa (RCC) ,ambacho kilikuwa maalumu kwa suala la hifadhi ya mazingiraambapo amekitaka  Kikosi cha usalama barabarani kiandae mpango wa ukaguzi wa magari ya wanafunzi kila Jumamosi, na yale yasiyo na sifa yaondolewe barabarani.

Sadiki amesema Serikali ilisikitishwa na vifo vya watu wasio na hatia ,kwani pia katika ajali hiyo mkoa wake uliguswa kwa kupoteza watoto 14.

Aidha amemtaka Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Hamisi Issa kusimamia kikamilifu ukaguzi huo ili kuepuka udanganyifu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu