Serikali mkoani Kilimanjaro yaanza rasmi zoezi la kukagua magari yanayo safirisha wanafunzi.

In Kitaifa
   Serikali mkoani Kilimanjaro imeanza zoezi rasmi la operesheni maalumu ya kukagua magari yanayosafirisha wanafunzi wa shule za mkoa huo ili kujiridhisha kama yana ubora ambao unastahili katika kutoa huduma  ambayo ni salama na bora kama yalivyo maelekezo ya sheria za usafirishaji.
Akizungumza na vyombo vya habari  mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Saidi Meck Sadiki amesema katika kuhakikisha zoezi hilo linatekelezwa ipasavyo,wameshirikisha jeshi la polisi ,temesa na mamlaka ya usafiri wa majini na nchi kavu(Sumatra) na kwamba litafanyika kila jumaosi na jumapili,ili kutoathi masomo kwa wanafunzi.
Kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro Hamisi Issah amesema katika zoezi hilo wanakagua ,uzima wa gari,ikiwemo ,rangi,mikanda,viti na mfumo wa breki,na kwamba wanapogundua gari lenye ubovu,wana liondoa namba zake,kisha kumwagiza mmiliki wake akalitengeneze ndipo aruhusiwe kuendelea na usafirishaj.
Nae afisa wa mfawidhi wa Sumatra mkoani Kilimanjaro Johns Makwale,amesema licha ya wamiliki kuwa na nyaraka muhimu za kuwaruhusu kufanya biashara ya usafirishaji ,baadhi ya magari yamegundulika kuwa na kasoro ndogo ndogo,ikiwemo uchakavu wa viti pamoja na kutokupigwa rangi iliyopendekezwa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu