Serikali ya awamu ya tano imejipanga kuhakikisha miradi mikubwa inatekelezwa kama ilivyoaidiwa.

In Kitaifa
Raisi wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania mh.dkt John Magufuli amewahakikishia wananchi wa mkoa wa pwani kuwa serikali ya awamu ya tano imejipanga kuhakikisha miradi mikubwa ya maendeleo yenye manufaa kwa mkoa huo na taifa kwa ujumla linatekelezwa kama ilivyoahidi.
Mh Raisi John magufuli amesema hayo katika mkutano wa hadhara uluofanyika katika uwanja wa bwawani mjini kibaha akiwa katika ziara ya kwanza katika ziara yake ya kikazi ya siku tatu mkoani pwani.
Dkt Magufuli ameitaja miradi hiyo ikiwa ni ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kisasa(standard gauge)ambayo imeanzwa kujengwa,ujenzi wa barabara ya njia sita kati ya dar-es-salaam na chalinze yenye urefu wa kilomita 128,ujenzi wa bandari kavu ya ruvu itakayo pokea mizigo kutoka katika banadari ya dar-es-salaamu na ujenzi wa mradi wa umeme katika maporomoko yam to rufiji amabo mipango ya kushirikiana na Ethopia imeanza.
Amebainisha pamoja na kutekeleza miradi hiyo serikali ya awamu ya tano itaendelea kuchukua hatua dhidi ya watu  waliohujumu taifa ikiwemo kujihusisha na vitendo vya wizi na rushwa,na aitakatishwa tama na watu wanao lalamika na  wanaobeza juhudi hizo.
Mapema akitoa taarifa ya maendeleo ya mkoa wa pwani,mkuu wa mkoa mhuhandisi Evarest ndikilo amesema kuwa mkoa huo unajumla ya viwanda 371 ikiwemo viwanda 9 vikubwa  na kwamaba ujenzi wa viwanda hivyo unaendelea katika hatua mbali mbali.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu