Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, imekataa wito wa Umoja wa Mataifa wa kuitaka serikali ya Kinshasa, kuanzisha uchunguzi wa kina na wa Kimataifa kuhusu machafuko yanayoendelea katika majimbo ya Kasai na Kasai ya Kati.

In Kimataifa

Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, imekataa wito wa Umoja wa Mataifa wa kuitaka serikali ya Kinshasa, kuanzisha uchunguzi wa kina na wa Kimataifa kuhusu machafuko yanayoendelea katika majimbo ya Kasai na Kasai ya Kati.

Majimbo hayo mawili yameendelea kushuhudia mauaji tangu mwaka 2015 baada ya kuanza kwa makabiliano kati ya wanajeshi wa serikali na waasi wa Kamwina Nsapu.

Umoja wa Mataifa unasema machafuko hayo yamesababisha vifo vya watu zaidi ya 400, huku wengine Milioni 1.3 wakiyakimbia makwao.

Hata hivyo, Mashirika ya kiraia yanaeleza kuwa watu huenda zaidi ya watu 3,000 wameuawa kutokana na mauaji hayo.

Mkuu wa Tume ya Haki za binadamu katika Umoja huo Zeid Ra’ad Al Hussein, amesema ameipa serikali ya Kinshasa siku mbili kuanzisha uchunguzi huo.

Hata hivyo Waziri anayeshughulikia maswala ya Haki nchini humo Marie-Ange Mushobekwa, amesema hakuna anayeweza kulipagia taifa hilo huru, jambo la kufanya.

Wiki hii, Marekani ilitia wito kwa Umoja wa Mataifa kuanza kufanya uchunguzi wa mauaji ya watalaam wake wawili waliouawa katika jimbo hilo mwezi Machi.

Serikali ya DRC tayari, imefungua kesi dhidi ya washukiwa waliokamatwa kuhusiana na kifo cha watalaam hao Michael Sharp na Zaida Catalan.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu