Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, imekataa wito wa Umoja wa Mataifa wa kuitaka serikali ya Kinshasa, kuanzisha uchunguzi wa kina na wa Kimataifa kuhusu machafuko yanayoendelea katika majimbo ya Kasai na Kasai ya Kati.

In Kimataifa

Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, imekataa wito wa Umoja wa Mataifa wa kuitaka serikali ya Kinshasa, kuanzisha uchunguzi wa kina na wa Kimataifa kuhusu machafuko yanayoendelea katika majimbo ya Kasai na Kasai ya Kati.

Majimbo hayo mawili yameendelea kushuhudia mauaji tangu mwaka 2015 baada ya kuanza kwa makabiliano kati ya wanajeshi wa serikali na waasi wa Kamwina Nsapu.

Umoja wa Mataifa unasema machafuko hayo yamesababisha vifo vya watu zaidi ya 400, huku wengine Milioni 1.3 wakiyakimbia makwao.

Hata hivyo, Mashirika ya kiraia yanaeleza kuwa watu huenda zaidi ya watu 3,000 wameuawa kutokana na mauaji hayo.

Mkuu wa Tume ya Haki za binadamu katika Umoja huo Zeid Ra’ad Al Hussein, amesema ameipa serikali ya Kinshasa siku mbili kuanzisha uchunguzi huo.

Hata hivyo Waziri anayeshughulikia maswala ya Haki nchini humo Marie-Ange Mushobekwa, amesema hakuna anayeweza kulipagia taifa hilo huru, jambo la kufanya.

Wiki hii, Marekani ilitia wito kwa Umoja wa Mataifa kuanza kufanya uchunguzi wa mauaji ya watalaam wake wawili waliouawa katika jimbo hilo mwezi Machi.

Serikali ya DRC tayari, imefungua kesi dhidi ya washukiwa waliokamatwa kuhusiana na kifo cha watalaam hao Michael Sharp na Zaida Catalan.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu