Serikali yajipanga kukabiliana na matumizi mabaya ya mitandao.

In Kitaifa
Serikali imesema inajipanga kukabiliana na matumizi mabaya ya mtandao ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua za kisheria wanaotumia vibaya.
Akizungumza katika majadiliano ya usalama wa mitandao ya kijamii kati ya Tanzania na China, Naibu Waziri wa Wizara wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Injinia Edwin Ngonyani amesema serikali itawachukulia hatua kali wanaotumia vibaya mitandao ya kijamii, wakiwamo wanaotuma ujumbe wenye dhamira ya kuwachafua wengine.
Injinia Ngonyani amesema kuwa Tanzania bado ipo nyuma sana katika usimamizi wa mitandao ya kijamii tofauti na china mbayo imefanikiwa kwa kiasi kikubwa.
Naibu Waziri wa Udhibiti wa mtandao wa China, Ren Xianliang amesema nchi yao imefanikiwa kwa kiwango kikubwa katika kudhibiti matumizi ya usalama wa mtandao, kwa kuwa walianzisha mtandao wao ambao umekua unasaidia kufuatilia masuala ya nchi yao vikiwamo vivutio mbalimbali ambavyo huwashawishi na kutoa hamasa kwa wananchi wengi kuweza kutumia mtandao huo.
Aidha amesema pia china imekuwa ikifanya uhamasishaji kupitia vyombo vya habari kwa kuandaa vipindi maaalum kwa ajili ya kutoa elimu kwa wananchi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu