Serikali yaonyesha dhamira kutumia lugha ya kiswahili

In Kitaifa

Serikali ina dhamira ya dhati katika kuendeleza na kutumia lugha ya Kiswahili katika shughuli mbalimbali za kitaifa na kimataifa.

Aidha, walimu na wataalamu wa lugha ya Kiswahili nchini wametakiwa kuchangamkia fursa ya kukua kwa lugha hiyo katika nchi zinazohitaji wataalamu wa lugha hiyo.

Hayo yamebainishwa na Waziri Mkuu, Kassimu Majaliwa wakati wa uzinduzi wa Kamusi Kuu ya Kiswahili, kwenye ukumbi wa Bunge  Mjini Dodoma.

Amesema katika kuendeleza na kukitumia Kiswahili, serikali imekusudia kuwa na miundombinu imara ya kuwezesha upatikanaji wa wakalimani, walimu wa Kiswahili kwa wageni na wafasiri wa kutosha kukidhi mahitaji yanayoongezeka kwa kasi.

Katibu Mtendaji wa BAKITA, Dk Seleman Sewangi alisema baraza limefikia hatua hiyo baada ya kuwapo kwa hazina ya misamiati mipya iliyofanyiwa utafiti.

Kamusi Kuu ya Kiswahili imeandaliwa na Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA) na kampuni ya uchapishaji ya Longhom ya Kenya.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu