Serikali yaonyesha dhamira kutumia lugha ya kiswahili

In Kitaifa

Serikali ina dhamira ya dhati katika kuendeleza na kutumia lugha ya Kiswahili katika shughuli mbalimbali za kitaifa na kimataifa.

Aidha, walimu na wataalamu wa lugha ya Kiswahili nchini wametakiwa kuchangamkia fursa ya kukua kwa lugha hiyo katika nchi zinazohitaji wataalamu wa lugha hiyo.

Hayo yamebainishwa na Waziri Mkuu, Kassimu Majaliwa wakati wa uzinduzi wa Kamusi Kuu ya Kiswahili, kwenye ukumbi wa Bunge  Mjini Dodoma.

Amesema katika kuendeleza na kukitumia Kiswahili, serikali imekusudia kuwa na miundombinu imara ya kuwezesha upatikanaji wa wakalimani, walimu wa Kiswahili kwa wageni na wafasiri wa kutosha kukidhi mahitaji yanayoongezeka kwa kasi.

Katibu Mtendaji wa BAKITA, Dk Seleman Sewangi alisema baraza limefikia hatua hiyo baada ya kuwapo kwa hazina ya misamiati mipya iliyofanyiwa utafiti.

Kamusi Kuu ya Kiswahili imeandaliwa na Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA) na kampuni ya uchapishaji ya Longhom ya Kenya.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu