Serikali yataifisha kiwanda cha ngozi.

In Kitaifa

Serikali imekitaifisha kiwanda cha kusindika ngozi cha Mwanza Tanneries kilichopo eneo la viwanda Ilemela mkoani Mwanza,baada ya wamiliki wake kushindwa kukiendeleza kuanzia mwaka 1998 hadi sasa,huku ikibaini kuwepo kwa udanganyifu wa umiliki wa kiwanda hicho uliodaiwa kufanywa nakampuni ya Quality group.

Uamuzi huo umetangazwa na mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella mbele ya wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa huo,wakiwemo pia wawakilishi wa kampuni ya Caspian na Quality group zilizoshindwa kutekeleza masharti ya mkataba wa kukiendeleza kiwanda hicho.

Kiwanda hicho awali kilikuwa kikimilikiwa na kampuni ya Africa Tanneries kisha kubadilishwa umiliki wake kwenda kwa kampuni ya Kasco ambayo na yenyewe inadaiwa imebadilisha umiliki wake kwa kampuni ya Quality group ambayo inadaiwa imeshindwa kukiendeleza.

Kampuni za quality group na Kasco zimekuwa kwenye mgogoro wa muda mrefu juu ya umiliki wa kiwanda hicho,huku kila mmoja akidai kuwa ndiye mmiliki halali,hadi serikali ilipoamua kukata mzizi wa fitina baada ya kuchukua hatua ya kukifunga na kukitaifisha hadi hapo mwafaka utakapopatikana.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu