Serikali yatangaza punguzo kubwa la bei za dawa.

In Kitaifa
Serikali yatangaza punguzo kubwa la bei za dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara baada ya kuanza utaratibu wa bohari kuu ya dawa kununua dawa moja kwa moja kutoka viwandani badala ya kupitia kwa mawakala.
Akitangaza utekelezaji wa maelekezo ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli yanayolenga kuunga mkono jitihada zake katika kujenga uchumi wa viwanda bohari kuu ya dawa kununua dawa zenye ubora kutoka kwa wazalishaji.
Akizungumza jijini Dar es Salaam waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Mh. Ummy Mwalimu amesema gharama za kununua dawa zitapungua kwa asilimia 15 hadi 80 ikiwemo dawa ya chanjo ya homa ya ini.
Aidha,Mh. Ummy Mwalimu licha ya kuziagiza halmashauri zahanati vituo vya afya hospitali za serikali kutumia bei elekezi ya dawa zilizotolewa na wizara ya afya kupitia orodha ya bei kwa bohari kuu ya dawa MSD tayari amesema serikali imeingia mikataba na wazalishaji 73.
Kwa upande wake mkurugenzi mkuu wa bohari kuu ya dawa MSD Laurean Rugambwa Bwanakunu amekabidhi  kitabu kipya cha bei za dawa zenye punguzo ambazo mabadiliko ya bei yameanza kutumika julai mosi mwaka huu na kuwakikishia  wananchi kuwa watafuata maelekezo ya serikali kama ilivyoagiza.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu