Serikali yatenga sh18.1 bilioni kwa ajili ya kujenga na kukarabati mahakama mbalimbali Nchini.

In Kitaifa

Serikali kupitia Wizara ya Katiba na Sheria kwa Mwaka 2017/18 imetenga Sh18.1 bilioni kwa ajili ya kujenga na kukarabati mahakama mbalimbali nchini.

Kauli hiyo ilitolewa bungeni na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angela Kairuki alipokuwa akijibu swali la nyongeza lililoulizwa na Mbunge wa Mlalo, Rashid Shangazi(CCM).

Kairuki amesema azma ya Serikali ni kusogeza huduma za mahakama karibu na wananchi na kwamba katika mwaka wa fedha 2016/17 zilitengwa Sh 46.5 bilioni ambazo zimefanya kazi kubwa.

Amesema mahakama ambazo zipo kwenye utaratibu wa kukarabatiwa, ni Mahakama Kuu ya Tanga na Dar es salaam na kuanza ujenzi katika Mahakama Kuu ya Mara na Kigoma.

Katika swali la msingi la Mbunge wa Njombe Mjini (CCM), Edward Mwalongo alitaka kujua kama Serikali itakuwa tayari kukarabati Mahakama za Mwanzo za Mahenye na Igomonyi ili wananchi waweze kupata huduma hiyo karibu.

Akijibu swali hilo Kairuki amesema moja ya changamoto kubwa zinazoikabili Mahakama ni uchakavu wa miundombinu na ukosefu wa majengo ya kutosha.

Amesema mpango uliopo ni kujenga majengo mapya na siyo kukarabati yaliyopo hasa ikizingatiwa kuwa majengo yaliyoombewa na mbunge yapo kwenye hifadhi za barabara na pia ujenzi wa Mahakama ya Mwanzo Njombe ni miongoni mwa miradi ya kipaumbele.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu