Serikali yateua Kamati Maalumu kukagua utendaji wa viwanda.

In Kitaifa

Serikali imeteua kamati maalumu yenye kushirikisha wataalamu pamoja na wakuu wa mikoa wa kila mkoa, itakayozunguka kukagua utendaji wa viwanda vilivyobinafsishwa, na kisha ndani ya siku 15 itatoa maamuzi.

Imesema viwanda watakavyoshughulika navyo ni vile vilivyobinafsishwa na ambavyo havifanyi kazi, lakini pia kuhakikisha uzalishaji wa kiwanda husika kama ndio ulioruhusiwa.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage amesema hayo jijini Dar es Salaam ,na kuongeza kuwa wapo waliopewa viwanda kwa shilingi moja na wengine kwa Sh. milioni 10, vingine vikifanya kazi, vingine vikiwa havifanyi kazi iliyokusudiwa na vingine kutokufanya kazi kabisa.

Amesema Kamati hiyo itafuatilia na tayari ameandika barua kwa wakuu wote wa mikoa nchini, na kupewa hadidu za rejea ili waweze kupitia kiwanda kimojakimoja kuhakikisha utendaji kazi wake.

Aidha amesema lengo la kubinafsisha viwanda ni ili vizalishe bidhaa ambazo zitatumika nchini na nyingine ziweze kuuzwa nje ya nchi na kuleta fedha za kigeni, vifanye kazi viweze kutoa ajira kwani asilimia 65 ya idadi ya watu nchini n I vijana na wengi wao hawana ajira.

Ametoa wito kwa wakuu wa mikoa, kukagua kiwanda kimoja baada ya kingine na hata kuhoji umiliki, hivyo mhusika anatakiwa kuwa na nyaraka stahiki, kwani ubinafsishaji dhamira yake kubwa ilikuwa ni kuwepo kwa ajira.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu