Serikali yavunja Bodi ya Baraza la Taifa la Hifadhi ya Usimamizi wa Mazingira (NEMC)

In Kitaifa
SERIKALI imevunja Bodi ya Baraza la Taifa la Hifadhi ya Usimamizi wa Mazingira (NEMC), sambamba na kufanya mabadiliko ya uongozi huku watumishi wanne wakisimamishwa kazi kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazowakabili.
Akizungumza  na waandishi wa habari, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba amesema hatua hiyo imetokana na kukithiri kwa malalamiko ya wananchi na wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.
Makamba amesema ameamua  kutengua uteuzi wa wajumbe wote saba wa Bodi ya NEMC ili baadaye ateuwe  wajumbe wapya ambao wataenda na kasi na ari inayohitajika sasa katika kuelekea uchumi wa viwanda.
Hata hivyo amesema  Mwenyekiti wa Bodi ambaye mamlaka yake ya uteuzi ni ya Rais, ataendelea kuwepo hadi hapo atakapoteuliwa mwingine na  amemteua Dk Elikana Kalumanga, kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NEMC hadi hapo rais atakapofanya uteuzi kwa nafasi hiyo.
Kalumunga ni Mhadhiri katika Taasisi ya Usimamizi na Tathmini ya Rasilimali Asili, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Waziri Makamba amesema ili kuboresha utendaji wa NEMC, amefanya mabadiliko ya baadhi ya wakurugenzi na wakuu wa kanda, kwa Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa NEMC, Charles Wangwe kumrejesha Wizara ya Fedha na Mipango atakapopangiwa kazi kulingana na mahitaji ya serikali.
Nafasi hiyo itakaimiwa na Adam Minja kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu