Sheikh Mkuu wa Tanzania Mufti Abubakar Zubeir amesisitiza haja ya waumini wa madhehebu mbalimbali za dini hapa nchini kushikamana zaidi, ili kulinda na kudumisha amani na mshikamano wa kitaifa uliopo nchini.

In Kitaifa
Sheikh Mkuu wa Tanzania Mufti Abubakar Zubeir amesisitiza haja ya waumini wa madhehebu mbalimbali za dini hapa nchini kushikamana zaidi, ili kulinda na kudumisha amani na mshikamano wa kitaifa uliopo nchini.
Mufti Abubakar Zubeir ametoa msisitizo huo jijini Dar es salaam katika hafla ya futari iliyowakutanisha waumini wa madhehebu tofauti ya dini, iliyoandaliwa kwa pamoja na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania BAKWATA kwa kushirikiana na Jumuiya ya ‘Khoja Shia Ithnaasheri’ mkoani Dar es salaam.
Amesema kwa mujibu wa mafundisho ya vitabu vyote vya dini, binadamu wote ni ndugu kwa sababu wanatokana na asili moja, licha ya binadamu hao kuwa na dini na madhehebu tofauti.
Hafla hiyo iliyopewa jina la ‘Interfaith Iftar’ ilihudhuriwa na waumini wa madhehebu mbalimbali ya dini wakiwemo viongozi wa kisiasa na mabalozi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu