Shirika la Afya duniani (WHO) limetangaza kutokea kwa milipuko miwili ya ugonjwa wa polio nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, miezi michache baada ya nchi hiyo kukumbwa na ugonjwa mwengine hatari wa Ebola, ambao ulisababisha kifo cha watu kadhaa kaskazini mwa DRC.

In Kimataifa
Shirika la Afya duniani (WHO) limetangaza kutokea kwa milipuko miwili ya ugonjwa wa polio nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, miezi michache baada ya nchi hiyo kukumbwa na ugonjwa mwengine hatari wa Ebola, ambao ulisababisha kifo cha watu kadhaa kaskazini mwa DRC.
Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema uwepo wa maambukizi ya ugonjwa wa polio umebainika upo katika maeneo ambayo hawakupata kinga ya kutosha nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Inaaminiwa kuwa maambukizi ya polio yanawashambulia zaidi vijana na athari zake ni kupooza kwa kudumaa kwa baadhi ya viongo vya mwili vya binadamu.
Nchi ambazo zinakabiliwa hasa na ugonjwa huu licha ya kuwepo kwa kampeni nyingi za kuutokomeza ugonjwa huu ni Nigeria, Pakistan na Afghanistan.
Shirika la Afya Duniani linabaini kwamba kuna hatari kubwa ya ugonjwa huo kusambaa katika baadhi ya maeneo nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu