Shirika la Afya duniani (WHO) limetangaza kutokea kwa milipuko miwili ya ugonjwa wa polio nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, miezi michache baada ya nchi hiyo kukumbwa na ugonjwa mwengine hatari wa Ebola, ambao ulisababisha kifo cha watu kadhaa kaskazini mwa DRC.

In Kimataifa
Shirika la Afya duniani (WHO) limetangaza kutokea kwa milipuko miwili ya ugonjwa wa polio nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, miezi michache baada ya nchi hiyo kukumbwa na ugonjwa mwengine hatari wa Ebola, ambao ulisababisha kifo cha watu kadhaa kaskazini mwa DRC.
Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema uwepo wa maambukizi ya ugonjwa wa polio umebainika upo katika maeneo ambayo hawakupata kinga ya kutosha nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Inaaminiwa kuwa maambukizi ya polio yanawashambulia zaidi vijana na athari zake ni kupooza kwa kudumaa kwa baadhi ya viongo vya mwili vya binadamu.
Nchi ambazo zinakabiliwa hasa na ugonjwa huu licha ya kuwepo kwa kampeni nyingi za kuutokomeza ugonjwa huu ni Nigeria, Pakistan na Afghanistan.
Shirika la Afya Duniani linabaini kwamba kuna hatari kubwa ya ugonjwa huo kusambaa katika baadhi ya maeneo nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu