Shirika la Kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF limeonya kwamba watoto takriban milioni tano nchini Iraq wanahitaji msaada wa haraka wa kibinadamu.

In Kimataifa

Shirika la Kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF limeonya kwamba watoto takriban milioni tano nchini Iraq wanahitaji msaada wa haraka wa kibinadamu.

Shirika hilo limesema watoto wa nchi hiyo hususan wale wote walio katika mji wa Mosul, ambako majeshi ya Iraq yanapambana vikali na wapiganaji wa Islamic state, wamejikuta katika ghasia na umasikini usio na mwisho.

Takwimu zilizooneshwa na UNICEF zinaonesha kuwa nusu ya wagonjwa wanaotibiwa katika vituo vya watu wenye maradhi ya wasiwasi na kuchanganyikiwa kutokana na hofu, (magonjwa mabaya ya akili) magharibi mwa Mosul ni watoto.

Kwa mujibu wa ripoti, watoto wapatao laki nane nchini Iraq kote, wamepoteza mzazi japo mmoja.

Mashirika ya misaada yanasema fedha zaidi zinahitajika haraka kuweza kusaidia kuwalinda watoto wa Iraq, kutokana na mapigano hayo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu