Shisha yapigwa marufuku Mkoani Dodoma.

In Kitaifa

Serikali ya Mkoa wa Dodoma  imepiga marufuku uvutaji wa kilevi aina ya shisha unaoendelea kwenye mahoteli yote mkoani humo, ikisema ni sehemu ya madawa ya kulevya.
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa  wa Dodoma JORDAN RUGIMBANA jana  kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya siku ya kupiga vita dawa za kulevya duniani , ambayo yatafanyika leo mjini Dodoma ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa  Waziri Mkuu wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzani  KASSIM MAJALIWA.
Mkuu huyo ameongeza kusema  Mkoa wa Dodoma ni mojawapo ya mikoa ambayo imeathirika zaidi na madawa ya kulevya, kwa kuwa ina vijana wengi ambao wapo vyuoni hivyo ni walengwa wakubwa wa madawa hayo.
RUGIMBANA ameeleza kuwa mahoteli mengi yamekuwa na mtindo wa kuweka kilevi aina ya shisha kwa ajili ya kuwavutia wateja wao, na hivyo kukipiga marufuku kilevi hicho mkoani humo.

Naye mwakilishi wa kamishna jenerali wa tume ya kuthibiti madawa ya kulevya ambaye pia ni kamishna msaidizi wa kinga, tiba na utafiti Dk, CASSIAN NYANDINDI, amesema kuwa kuna njia kuu tatu za kupambana na madawa ya kulevya ambazo hutumika duniani kote ambazo ni kuwakamata na kuwathibiti wasambazaji na wauzaji wa dawa za kulevya, kutoa elimu ya madhara ya dawa za kulevya kwa watu ambao bado hawajaingia kwenye matumizi na kutoa fursa ya tiba kwa waathirika wa dawa za kulevya ili kupunguza madhara yaliyotokana na madawa ya kulevya.

Maadhimisho hayo ya siku ya kupiga vita dawa za kulevya duniani yatafanyika  kitaifa mkoani Dodoma, ambapo  kauli mbiu   inasema tuwasikilize na kuwashauri vijana na watoto ili kuwaepusha na dawa za kulevya.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu