Shisha yapigwa marufuku Mkoani Dodoma.

In Kitaifa

Serikali ya Mkoa wa Dodoma  imepiga marufuku uvutaji wa kilevi aina ya shisha unaoendelea kwenye mahoteli yote mkoani humo, ikisema ni sehemu ya madawa ya kulevya.
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa  wa Dodoma JORDAN RUGIMBANA jana  kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya siku ya kupiga vita dawa za kulevya duniani , ambayo yatafanyika leo mjini Dodoma ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa  Waziri Mkuu wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzani  KASSIM MAJALIWA.
Mkuu huyo ameongeza kusema  Mkoa wa Dodoma ni mojawapo ya mikoa ambayo imeathirika zaidi na madawa ya kulevya, kwa kuwa ina vijana wengi ambao wapo vyuoni hivyo ni walengwa wakubwa wa madawa hayo.
RUGIMBANA ameeleza kuwa mahoteli mengi yamekuwa na mtindo wa kuweka kilevi aina ya shisha kwa ajili ya kuwavutia wateja wao, na hivyo kukipiga marufuku kilevi hicho mkoani humo.

Naye mwakilishi wa kamishna jenerali wa tume ya kuthibiti madawa ya kulevya ambaye pia ni kamishna msaidizi wa kinga, tiba na utafiti Dk, CASSIAN NYANDINDI, amesema kuwa kuna njia kuu tatu za kupambana na madawa ya kulevya ambazo hutumika duniani kote ambazo ni kuwakamata na kuwathibiti wasambazaji na wauzaji wa dawa za kulevya, kutoa elimu ya madhara ya dawa za kulevya kwa watu ambao bado hawajaingia kwenye matumizi na kutoa fursa ya tiba kwa waathirika wa dawa za kulevya ili kupunguza madhara yaliyotokana na madawa ya kulevya.

Maadhimisho hayo ya siku ya kupiga vita dawa za kulevya duniani yatafanyika  kitaifa mkoani Dodoma, ambapo  kauli mbiu   inasema tuwasikilize na kuwashauri vijana na watoto ili kuwaepusha na dawa za kulevya.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu