siku 40 zasalia Uchaguzi Mkuu ufanyike Kenya.

In Kimataifa

Huku zikiwa zimesalia siku 40 kwa uchaguzi mkuu kufanyika, wanasiasa wako mbioni kujipigia debe na kuwarai wananchi kuwapigia kura ifikapo Agosti nane mwaka huu.

Katika karne hii ya mitando ya kijamii, wanasiasa hawa na wafuasi wao wametumia fursa hii kueneza kampeni zao kote kote.

Waziri wa usalama wa ndani wa Kenya, Joseph Nkaisery amewaonya wananchi wa Kenya wakiwemo wanasiasa dhidi ya kutumia mitandao ya kijamii kueneza chuki.

Badala yake, Nkaisery amewaomba wananchi kutumia simu zao za mkononi kuwarekodi wanasiasa wanaoneza ukabila na kuwachochea wananchi, na kusambaza video hizo pamoja na sauti ili kusaidia wanasiasa hao kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Pia amewataka wanasiasa kufanya kampeni zao kwa amani bila kueneza chuki ili uchaguzi ufanyike na umalizike  kwa wakati.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu