siku 40 zasalia Uchaguzi Mkuu ufanyike Kenya.

In Kimataifa

Huku zikiwa zimesalia siku 40 kwa uchaguzi mkuu kufanyika, wanasiasa wako mbioni kujipigia debe na kuwarai wananchi kuwapigia kura ifikapo Agosti nane mwaka huu.

Katika karne hii ya mitando ya kijamii, wanasiasa hawa na wafuasi wao wametumia fursa hii kueneza kampeni zao kote kote.

Waziri wa usalama wa ndani wa Kenya, Joseph Nkaisery amewaonya wananchi wa Kenya wakiwemo wanasiasa dhidi ya kutumia mitandao ya kijamii kueneza chuki.

Badala yake, Nkaisery amewaomba wananchi kutumia simu zao za mkononi kuwarekodi wanasiasa wanaoneza ukabila na kuwachochea wananchi, na kusambaza video hizo pamoja na sauti ili kusaidia wanasiasa hao kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Pia amewataka wanasiasa kufanya kampeni zao kwa amani bila kueneza chuki ili uchaguzi ufanyike na umalizike  kwa wakati.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu