Kikosi cha Simba leo kimewasili salama Mbeya baada ya
kuondoka leo Dar es Salaam.
Simba ilikwea pipa asubuhi ili kuwahi kufanya maandalizi dhidi
ya mechi mbili zitakazopigwa Mbeya ambapo itaanza Jumatano,
Juni 24 dhidi ya Mbeya City Uwanja wa Sokoine.
Simba itawafuata Mbeya City ikiwa na kumbukumbu za
ushindi wa mabao 3-0 mbele ya Mwadui FC kwenye mchezo
wao waliocheza Uwanja wa Taifa huku Mbeya City ikiwa na
kumbukukumbu ya kufungwa bao 1-0 na Alliance.