Simbachawene ashauri halmashauri zilizopo Mkoani Dodoma kutumia Benki ya DCB.

In Kitaifa

WAZIRI wa nchi ofisi ya Rais (Tamisemi) George Simbachawene amezishauri Halmashauri zilizoko kwenye Mkoa wa Dodoma ,kuitumia Benki ya DCB kupitishia fedha zake za kuwakopesha vijana na wanawake ili fedha hizo ziweze kutumiwa na kurejeshwa kwa wakati.

Simbachawene ametoa kauli hiyo Mjini Dodoma  wakati akizindua tawi jipya la benki hiyo, ambalo ni la kwanza kuwa nje ya mkoa wa Dar es Salaam.

Amesema kumekuwa na changamoto nyingi zinazozikabili halmashauri katika urejeshwaji wa fedha, zinazotolewa kwenye vikundi vya vijana na wanawake hivyo akawashauri kuitumia benki hiyo kupitishia fedha hizo, ili ziweze kukopeshwa kwa masharti nafuu na kurejeshwa kwa wakati

Naye mkurugenzi mtendaji wa benki ya DCB, Edmund Mkwawa amesema kuwa benki hiyo imejipanga kukopesha fedha kiasi cha sh. 105 bilion kwa wajasiriamlai na wafanyabiashara wakubwa mkoani Dodoma ambapo katika Wilaya za Mkoa huo,kutakuwa na mawakala zaidi ya 90 ambao watakuwa wanatoa huduma kwa wananchi walioko Wilayani.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu