Sirro awaomba msaada viongozi wa dini.

In Kitaifa

Mkuu wa jeshi la polisi nchini IGP simon siro, amewaomba viongozi wa dini na wanasiasa mkoani Iringa, kushirikiana katika kutokomeza vitendo vya ulawiti na ubakaji, ambavyo vinazidi kushamiri mkoani humo.

IGP Siro ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari, katika ziara yake ya kikazi ya siku moja mkoani humo.

Amesema ili vitendo hivyo vitokomezwe ni lazima elimu izidi kutolewa kwa jamii, hususani masuala ya imani za kishirikina ambayo yametajwa kuwa chanzo kikubwa cha kuchangia matukio hayo.

Aidha IGP Sirro amewasihi askari kufanya kazi kwa kuzingatia misingi ya sheria, bila kumuonea mtu yoyote kwakuwa hakuna mtu ambaye yupo juu ya sheria.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu