Somalia yasaini mkataba wa utulivu wenye lengo la kuimarisha Jeshi lake.

In Kimataifa

Somalia imesaini mkataba wa utulivu wenye lengo la kuimarisha jeshi lake na kufufua uchumi wake uliodorora.
Baada ya kusainiwa mkataba huo kati ya Somalia na mtandao wa kimataifa, Rais Mohammed Abdullahi Mohamed amesema katika mkutano wa mjini London Uingereza kwamba siku ya kusaini mkataba huo ni ya kihistoria kwa Somalia.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ambaye alikuwa miongoni mwa wenyeji wa hafla hiyo, amesema Somalia itakuwa na mafanikio.
Mkataba huo una lengo la kufanya kazi ya kuipatia msamaha wa madeni Somalia na kuisaidia kupambana na wapiganaji wa kundi la mitazamo mikali ya Kiislam al-Shabaab, ambalo kwa miaka kumi limekuwa likijaribu kuipindua serikali ya Somalia.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu