Spika aeleza jinsi Lissu alivyoshambuliwa.

In Kitaifa, Siasa

Spika wa Bunge Job Ndugai amesema kuwa, mwanasheria Mkuu wa Chadema na Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu, alishambuliwa kwa risasi kati ya 28 hadi 32, huku tano zikimpata mwilini.

Lissu alishambuliwa jana Alhamisi kabla hajashuka kwenye gari, baada ya kumaliza kikao cha Bunge na alipelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma kabla ya kusafirishwa saa sita usiku, kuelekea Hospitali ya Aga Khan ya Nairobi Kenya.

Akitoa taarifa ya tukio hilo kwenye kikao cha Bunge leo Ijumaa, Ndugai amesema risasi mbili zilimpata Lissu kwenye miguu, mbili tumboni na moja kwenye mkono.

Pia kumekuwepo na maswali mengi na mitizamo tofauti kwa baadhi ya watu, juu ya Tundu Lissu kupelekwa Nairobi kwa matibu, hili nalo mheshimiwa spika amelifafanua.

Baada ya kutokea tukio hilo pia baadhi ya wabunge kupitia mitandao ya kijamii, wamekuwa wakiandika mambo mbali mbali juu ya tukio hilo.

Hilo nalo mheshimiwa spika amelizungumzia, pamoja na kuelezea kiasi cha fedha kilichopatika kusaidia matibabu ya Lissu baada ya wabunge kukubali kutoa nusu ya posho zao za siku moja.

Wakati huo huo Marekani imeeleza kusikitishwa na tukio la kushambuliwa kwa risasi Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu.

Taarifa ya Ubalozi wa Marekani nchini iliyotolewa kupitia ukurasa wake wa Facebook imesema kuwa, Marekani inalaani kitendo hiki cha kipuuzi na cha kutumia nguvu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu