Spika wa Bunge ajiuzulu akipinga vitendo vya Serikali.

In Kimataifa

Spika wa Bunge la Ethiopia Abadula Gemeda, amejiuzulu nafasi hiyo ikiwa ni siku mbili kabla ya kufunguliwa kwa vikao vya bunge hilo.

Kwa mujibu wa tovuti maarufu ya Addis Standard, Gemeda amechukua uamuzi huo wikendi iliyopita kama ishara ya kupinga vitendo vya Serikali ya nchi hiyo, katika masuala ya ulinzi kwenye majimbo ya Oromia na Somali.

Sababu kuu imeelezwa kuwa ni ukosoaji wa namna ambavyo Serikali inavyotumia vikosi vya ulinzi katika maeneo hayo, wakati ambapo watu 50 wameripotiwa kufa na zaidi ya watu 150,000 wamepoteza makazi kutokana na mgogoro wa rasilimali unaohusisha ukabila.

Kabla hajawa Spika wa Bunge hilo tangu mwaka 2010, Gemeda aliwahi kuwa Gavana wa jimbo la Oromia na pia Waziri wa Ulinzi.

Spika mpya wa Bunge hilo anatarajiwa kuchaguliwa mara tu wabunge watakapokutana wiki hii.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu