Stella Manyanya awataka wanafunzi wote nchini, kusoma kwa bidii masomo ya sayansi

In Kitaifa

NAIBU Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Stella Manyanya amewataka wanafunzi wote nchini, kusoma kwa bidii masomo ya sayansi, teknolojia na ubunifu ili kuhakikisha ndoto ya Tanzania ya kuwa na uchumi wa kati kupitia viwanda na biashara inafanikiwa.

Amesema kuwa sayansi, teknolojia na ubunifu, ndio njia pekee itakayowezesha nchi kupata maendeleo kwa kasi na kupunguza utegemezi wa teknolojia.

Naibu Waziri amesema hayo jana katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Jangwani Dar es Salaam wakati wa kukabidhi bendera ya Taifa ,kwa wanafunzi saba wanaosoma masomo ya sayansi wanaokwenda kuiwakilisha nchi katika mashindano ya First Global Challenges nchini Marekani.

Shule zilizotoa wanafunzi watakaoshiriki mashindano hayo ni Jangwani, Benjamin Mkapa, Jamhuri, Feza, Azania na Kisutu ambapo amesema nchi inahitaji viwanda vinavyotumia teknolojia ya kisasa ili kuongeza ufanisi na kwamba roboti zilizoanza kubuniwa na vijana hao ndizo zitakazokuwa msingi wa viwanda hivyo.

Aidha, aliwahimiza wanafunzi wote kutoogopa masomo ya sayansi kwa kuwa ni rahisi na pia kuna uhitaji mkubwa wa wataalamu katika fani mbalimbali.

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu