Stella Manyanya awataka wanafunzi wote nchini, kusoma kwa bidii masomo ya sayansi

In Kitaifa

NAIBU Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Stella Manyanya amewataka wanafunzi wote nchini, kusoma kwa bidii masomo ya sayansi, teknolojia na ubunifu ili kuhakikisha ndoto ya Tanzania ya kuwa na uchumi wa kati kupitia viwanda na biashara inafanikiwa.

Amesema kuwa sayansi, teknolojia na ubunifu, ndio njia pekee itakayowezesha nchi kupata maendeleo kwa kasi na kupunguza utegemezi wa teknolojia.

Naibu Waziri amesema hayo jana katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Jangwani Dar es Salaam wakati wa kukabidhi bendera ya Taifa ,kwa wanafunzi saba wanaosoma masomo ya sayansi wanaokwenda kuiwakilisha nchi katika mashindano ya First Global Challenges nchini Marekani.

Shule zilizotoa wanafunzi watakaoshiriki mashindano hayo ni Jangwani, Benjamin Mkapa, Jamhuri, Feza, Azania na Kisutu ambapo amesema nchi inahitaji viwanda vinavyotumia teknolojia ya kisasa ili kuongeza ufanisi na kwamba roboti zilizoanza kubuniwa na vijana hao ndizo zitakazokuwa msingi wa viwanda hivyo.

Aidha, aliwahimiza wanafunzi wote kutoogopa masomo ya sayansi kwa kuwa ni rahisi na pia kuna uhitaji mkubwa wa wataalamu katika fani mbalimbali.

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu