WHO: Stress hugharimu dola trilioni 1 kila mwaka.

In Afya, Kimataifa

Leo ni siku ya afya ya akili duniani, ambapo maudhui ni afya njema ya akili pahala pa kazi ili kuongeza tija.

Shirika la afya ulimwenguni WHO linasema kuwa, kiwewe na msongo wa mawazo husababisha kupungua kwa tija, na hivyo kuleta hasara ya dola trilioni moja kila mwaka duniani.

Takwimu za WHO zinaonyesha kwamba, zaidi ya watu milioni 300 ulimwenguni wanakabiliwa na kiwewe na msongo wa mawazo, miongoni mwao wakiwa ni wafanyakazi.

WHO inasema afya njema ya akili pahala pa kazi, ni jambo muhimu kwa kuzingatia kuwa kipindi kikubwa cha utu uzima mtu hukitumia akiwa kazini.

Hivyo WHO imesihi mataifa kutumia siku ya leo, kuangazia na kuhamasisha umuhimu wa afya ya akili ili kuimarisha afya hiyo.

Antenna imepiga story na Daktari Iman Nkolela kutoka……na hapa anaelezea juu ya tatizo hili la afya ya akili.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu