WHO: Stress hugharimu dola trilioni 1 kila mwaka.

In Afya, Kimataifa

Leo ni siku ya afya ya akili duniani, ambapo maudhui ni afya njema ya akili pahala pa kazi ili kuongeza tija.

Shirika la afya ulimwenguni WHO linasema kuwa, kiwewe na msongo wa mawazo husababisha kupungua kwa tija, na hivyo kuleta hasara ya dola trilioni moja kila mwaka duniani.

Takwimu za WHO zinaonyesha kwamba, zaidi ya watu milioni 300 ulimwenguni wanakabiliwa na kiwewe na msongo wa mawazo, miongoni mwao wakiwa ni wafanyakazi.

WHO inasema afya njema ya akili pahala pa kazi, ni jambo muhimu kwa kuzingatia kuwa kipindi kikubwa cha utu uzima mtu hukitumia akiwa kazini.

Hivyo WHO imesihi mataifa kutumia siku ya leo, kuangazia na kuhamasisha umuhimu wa afya ya akili ili kuimarisha afya hiyo.

Antenna imepiga story na Daktari Iman Nkolela kutoka……na hapa anaelezea juu ya tatizo hili la afya ya akili.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu