Sudan yapokea mualiko kutoka Marekani.

In Kimataifa

Sudan imepokea mualiko kutoka Marekani wa mafunzo ya pamoja ya kijeshi na Misri, ukiwa ni mualiko wa kwanza wa aina hiyo kwa zaidi ya miongo mitatu.

Mkuu wa jeshi la Sudan, Jenerali Emad al-Din Adawi ametangaza mualiko huo wa mazoezi ya pamoja yajulikanayo kama Bright Star yatakayofanyika nchini Misri, baada ya kukutana na maafisa wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani wiki hii.

Mkuu huyo wa jeshi la Sudan amesema mkutano wao umefungua mlango kwa mazungumzo zaidi ambayo yanaweza kurejesha tena mahusiano kati ya Marekani na Sudan.

Mnamo mwezi Julai Marekani iliahirisha kwa miezi mitatu uamuzi wake wa kuiondolea vikwazo vya kiuchumi Sudan juu ya rekodi yake ya haki za binadamu na masuala mengine.

Uchumi wa Sudan umeporomoka tangu Sudan Kusini kujitenga mnamo mwaka 2011, na kuondoka na thuluthi tatu ya mafuta yanayozalishwa, chanzo chake kikuu cha fedha za kigeni na mapato ya serikali.

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu