Sudan yapokea mualiko kutoka Marekani.

In Kimataifa

Sudan imepokea mualiko kutoka Marekani wa mafunzo ya pamoja ya kijeshi na Misri, ukiwa ni mualiko wa kwanza wa aina hiyo kwa zaidi ya miongo mitatu.

Mkuu wa jeshi la Sudan, Jenerali Emad al-Din Adawi ametangaza mualiko huo wa mazoezi ya pamoja yajulikanayo kama Bright Star yatakayofanyika nchini Misri, baada ya kukutana na maafisa wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani wiki hii.

Mkuu huyo wa jeshi la Sudan amesema mkutano wao umefungua mlango kwa mazungumzo zaidi ambayo yanaweza kurejesha tena mahusiano kati ya Marekani na Sudan.

Mnamo mwezi Julai Marekani iliahirisha kwa miezi mitatu uamuzi wake wa kuiondolea vikwazo vya kiuchumi Sudan juu ya rekodi yake ya haki za binadamu na masuala mengine.

Uchumi wa Sudan umeporomoka tangu Sudan Kusini kujitenga mnamo mwaka 2011, na kuondoka na thuluthi tatu ya mafuta yanayozalishwa, chanzo chake kikuu cha fedha za kigeni na mapato ya serikali.

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu