TAASISI isiyo ya Kiserikali ya Hope 4 Young Girls Tanzania imetoa msaada wa baiskeli 60, kwa wanafunzi wa kike wa shule za sekondari za wilaya ya Kisarawe kwa ajili ya kuwasaidia kupunguza tatizo la utoro shuleni kunakotokana na kuishi mbali na shule.

In Kitaifa
TAASISI isiyo ya Kiserikali ya Hope 4 Young Girls Tanzania imetoa msaada wa baiskeli 60, kwa wanafunzi wa kike wa shule za sekondari za wilaya ya Kisarawe kwa ajili ya kuwasaidia kupunguza tatizo la utoro shuleni kunakotokana na kuishi mbali na shule.
Baiskeli hizo 60 zilikabidhiwa kwa kwa Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Happiness Seneda katika sherehe za kilele za siku ya kimataifa ya Mtoto wa Afrika ambazo zilifanyika wilayani humo katika kata ya Msimbu .
Akizungumza wakati wa kukabidhi baiskeli hizo, Mkurugenzi wa taasisi hiyo Salama Kikudo, amesema walifikia uamuzi huo wa kutoa baiskeli hizo kwa wasichana wa Kisarawe baada ya utafiti mdogo waliofanya kuonyesha kuwepo kwa tatizo la utoro na mimba kwa wanafunzi wa kike ambao wanaishi mbali na shule.
Akizungumza katika kilele hicho cha siku ya kimataifa ya Mtoto wa Afrika na mara baada ya kukabidhiwa baiskeli hizo Mkuu wa wilaya aliipongeza taasisi ya Hope4 Young Girls Tanzania kwa msaada huo kwa wanafunzi wa shule za sekondari za kike wilayani kwake.
Kwa upande wake Ofisa Mradi wa ‘Umakini wa Masomo, Urahisi wa Kujifunza’ kutoka Hope 4 Young Girls Tanzania, Winnie Mbowe amesema mradi huo ni endelevu na unalenga kufikia sehemu mbalimbali nchi nzima na kwa kuanzia wameanzia mkoa wa Pwani ambao wameshafika Kibaha na Mkuranga ambako walitoa misaada ya aina mbalimbali.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu