TAASISI isiyo ya Kiserikali ya Hope 4 Young Girls Tanzania imetoa msaada wa baiskeli 60, kwa wanafunzi wa kike wa shule za sekondari za wilaya ya Kisarawe kwa ajili ya kuwasaidia kupunguza tatizo la utoro shuleni kunakotokana na kuishi mbali na shule.

In Kitaifa
TAASISI isiyo ya Kiserikali ya Hope 4 Young Girls Tanzania imetoa msaada wa baiskeli 60, kwa wanafunzi wa kike wa shule za sekondari za wilaya ya Kisarawe kwa ajili ya kuwasaidia kupunguza tatizo la utoro shuleni kunakotokana na kuishi mbali na shule.
Baiskeli hizo 60 zilikabidhiwa kwa kwa Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Happiness Seneda katika sherehe za kilele za siku ya kimataifa ya Mtoto wa Afrika ambazo zilifanyika wilayani humo katika kata ya Msimbu .
Akizungumza wakati wa kukabidhi baiskeli hizo, Mkurugenzi wa taasisi hiyo Salama Kikudo, amesema walifikia uamuzi huo wa kutoa baiskeli hizo kwa wasichana wa Kisarawe baada ya utafiti mdogo waliofanya kuonyesha kuwepo kwa tatizo la utoro na mimba kwa wanafunzi wa kike ambao wanaishi mbali na shule.
Akizungumza katika kilele hicho cha siku ya kimataifa ya Mtoto wa Afrika na mara baada ya kukabidhiwa baiskeli hizo Mkuu wa wilaya aliipongeza taasisi ya Hope4 Young Girls Tanzania kwa msaada huo kwa wanafunzi wa shule za sekondari za kike wilayani kwake.
Kwa upande wake Ofisa Mradi wa ‘Umakini wa Masomo, Urahisi wa Kujifunza’ kutoka Hope 4 Young Girls Tanzania, Winnie Mbowe amesema mradi huo ni endelevu na unalenga kufikia sehemu mbalimbali nchi nzima na kwa kuanzia wameanzia mkoa wa Pwani ambao wameshafika Kibaha na Mkuranga ambako walitoa misaada ya aina mbalimbali.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu