Takriban watu wanane wameuwawa katika dhoruba zilizoyakumba maeneo ya pwani ya magharibi hapo jana Jumatano, katika mji wa Cape Town Afrika Kusini, na kuleta mafuriko yaliyosababisha uharibifu mkubwa, pamoja na kulazimisha kufungwa kwa bandari ya Cape Town kwa mujibu wa mamlaka za nchini humo.

In Kimataifa

Takriban watu wanane wameuwawa katika dhoruba zilizoyakumba maeneo ya pwani ya magharibi hapo jana Jumatano, katika mji wa Cape Town Afrika Kusini, na kuleta mafuriko yaliyosababisha uharibifu mkubwa, pamoja na kulazimisha kufungwa kwa bandari ya Cape Town kwa mujibu wa mamlaka za nchini humo.

Mabadiliko hayo ya hali ya hewa yameharibu majengo, na kupelekea miti kadhaa kuanguka, huku nyumba 46,000 zikibaki bila ya umeme.

Dhoruba hizo pia zimesababisha vurugu katika mifumo ya usafiri baada ya huduma za ndege na reli kukabiliana na upepo na mafuriko.

Moto uliwaka katika maeneo kadhaa kutokana na radi, na kuathiri makaazi ya vibanda ya jamii maskini. Dhoruba hizo pia zimeleta ahueni katika eneo lililokuwa na ukame mkali, na upungufu wa maji tokea mwanzoni mwa mwaka huu.

Mkoa wa Western Cape hata hivyo unasema unahitaji mvua za muda mrefu kutokana na kwamba hifadhi yao ya maji imekuwa ya kiwango cha chini.

 

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu