Takriban watu wanane wameuwawa katika dhoruba zilizoyakumba maeneo ya pwani ya magharibi hapo jana Jumatano, katika mji wa Cape Town Afrika Kusini, na kuleta mafuriko yaliyosababisha uharibifu mkubwa, pamoja na kulazimisha kufungwa kwa bandari ya Cape Town kwa mujibu wa mamlaka za nchini humo.

In Kimataifa

Takriban watu wanane wameuwawa katika dhoruba zilizoyakumba maeneo ya pwani ya magharibi hapo jana Jumatano, katika mji wa Cape Town Afrika Kusini, na kuleta mafuriko yaliyosababisha uharibifu mkubwa, pamoja na kulazimisha kufungwa kwa bandari ya Cape Town kwa mujibu wa mamlaka za nchini humo.

Mabadiliko hayo ya hali ya hewa yameharibu majengo, na kupelekea miti kadhaa kuanguka, huku nyumba 46,000 zikibaki bila ya umeme.

Dhoruba hizo pia zimesababisha vurugu katika mifumo ya usafiri baada ya huduma za ndege na reli kukabiliana na upepo na mafuriko.

Moto uliwaka katika maeneo kadhaa kutokana na radi, na kuathiri makaazi ya vibanda ya jamii maskini. Dhoruba hizo pia zimeleta ahueni katika eneo lililokuwa na ukame mkali, na upungufu wa maji tokea mwanzoni mwa mwaka huu.

Mkoa wa Western Cape hata hivyo unasema unahitaji mvua za muda mrefu kutokana na kwamba hifadhi yao ya maji imekuwa ya kiwango cha chini.

 

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu