Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa jijini Dodoma
TAKUKURU, leo wamezungumza na wanahabari na kutoa
taarifa mbali mbali za matukio ya Rushwa jijini humo.
Moja ya taarifa iliyotolewa na mkuu wa taasisi hiyo mkoani
humo ndugu Sostheness Kibwengo, ni wananchi 13 kurudishiwa
mashamba yenye ukubwa wa hekari thelasini na nyumba mbili
zilizokuwa zimechukuliwa kinyemela na bwana Nelson Ndalu
aliyekuwa amewakopesha fedha kwa riba kubwa kinyume na
taratibu.