Tambwe na Chirwa kuikosa Njombe Mji Jumapili hii.

In Kitaifa, Michezo

 

Washambuliaji wa klabu ya Yanga Hamissi Tambwe na Obrey Chirwa, wataikosa mechi yao dhidi ya ya Njombe Mji mwishoni mwa wiki hii mchezo ambao utachezwa katika uwanja wa Saba Saba Njombe.

Wachezaji hao wote walianza mazoezi mepesi jana katika Uwanja wa Uhuru jiji Dar es Salaam chini ya uangalizi maalum wa Daktari, lakini imeonekana hawatakuwa tayari kwa mchezo ujao wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Mpaka sasa Tambwe na Chirwa wameondolewa rasmi kwenye Orodha ya kocha Mzambia Geroge Lwandamina, katika mchezo ujao wa Ligi Kuu dhidi ya wenyeji Njombe Mji Jumapili.

Majeruhi wengine ni kipa Benno Kakolanya na viungo Hussein Akilimali, na Geoffrey Mwashiuya ambao wote tayari wameanza mazoezi mepesi.

Yanga wanatarajiwa kusaka ushindi wa kwanza Jumamosi, katika jitihada za kutetea ubingwa wao wa Ligi Kuu watakapokuwa wageni wa timu iliyopanda Daraja msimu huu

Ikumbukwe mabingwa hao wa Ligi Kuu waliuanza msimu mpya vibaya baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 na Lipuli ya Iringa iliyopanda Ligi Kuu msimu huu pia.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu