Tambwe na Chirwa kuikosa Njombe Mji Jumapili hii.

In Kitaifa, Michezo

 

Washambuliaji wa klabu ya Yanga Hamissi Tambwe na Obrey Chirwa, wataikosa mechi yao dhidi ya ya Njombe Mji mwishoni mwa wiki hii mchezo ambao utachezwa katika uwanja wa Saba Saba Njombe.

Wachezaji hao wote walianza mazoezi mepesi jana katika Uwanja wa Uhuru jiji Dar es Salaam chini ya uangalizi maalum wa Daktari, lakini imeonekana hawatakuwa tayari kwa mchezo ujao wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Mpaka sasa Tambwe na Chirwa wameondolewa rasmi kwenye Orodha ya kocha Mzambia Geroge Lwandamina, katika mchezo ujao wa Ligi Kuu dhidi ya wenyeji Njombe Mji Jumapili.

Majeruhi wengine ni kipa Benno Kakolanya na viungo Hussein Akilimali, na Geoffrey Mwashiuya ambao wote tayari wameanza mazoezi mepesi.

Yanga wanatarajiwa kusaka ushindi wa kwanza Jumamosi, katika jitihada za kutetea ubingwa wao wa Ligi Kuu watakapokuwa wageni wa timu iliyopanda Daraja msimu huu

Ikumbukwe mabingwa hao wa Ligi Kuu waliuanza msimu mpya vibaya baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 na Lipuli ya Iringa iliyopanda Ligi Kuu msimu huu pia.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu