Tambwe na Chirwa kuikosa Njombe Mji Jumapili hii.

In Kitaifa, Michezo

 

Washambuliaji wa klabu ya Yanga Hamissi Tambwe na Obrey Chirwa, wataikosa mechi yao dhidi ya ya Njombe Mji mwishoni mwa wiki hii mchezo ambao utachezwa katika uwanja wa Saba Saba Njombe.

Wachezaji hao wote walianza mazoezi mepesi jana katika Uwanja wa Uhuru jiji Dar es Salaam chini ya uangalizi maalum wa Daktari, lakini imeonekana hawatakuwa tayari kwa mchezo ujao wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Mpaka sasa Tambwe na Chirwa wameondolewa rasmi kwenye Orodha ya kocha Mzambia Geroge Lwandamina, katika mchezo ujao wa Ligi Kuu dhidi ya wenyeji Njombe Mji Jumapili.

Majeruhi wengine ni kipa Benno Kakolanya na viungo Hussein Akilimali, na Geoffrey Mwashiuya ambao wote tayari wameanza mazoezi mepesi.

Yanga wanatarajiwa kusaka ushindi wa kwanza Jumamosi, katika jitihada za kutetea ubingwa wao wa Ligi Kuu watakapokuwa wageni wa timu iliyopanda Daraja msimu huu

Ikumbukwe mabingwa hao wa Ligi Kuu waliuanza msimu mpya vibaya baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 na Lipuli ya Iringa iliyopanda Ligi Kuu msimu huu pia.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu