Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo uchumi wake unakua kwa kasi kubwa mpaka kupelekea viongozi mbalimbali wa taasisi kubwa duniani kuja nchini kwa ajili ya kujione na kutaka kujua mengi zaidi

In Kitaifa

Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo uchumi wake unakua kwa kasi kubwa mpaka kupelekea viongozi mbalimbali wa taasisi kubwa duniani kuja nchini kwa ajili ya kujione na kutaka kujua mengi zaidi.

Hali hiyo imedhihirika mara baada ya Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Tao Zhang  kuwasili nchini kwa ziara ya kikazi na kupokelewa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip  Mpango pamoja na maafisa wengine waandamizi wa Serikali katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa  Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.

Aidha, akiwa nchini, Tao Zhang atafanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli Ikulu Jijini Dar Es Salaam kwa ajili ya kuona ni namna gani Tanzania na IMF zinashirikiana katika kuimarisha uchumi.

Hata hivyo, Zhang atawasilisha mtazamo wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kwa wadau hapa nchini kwa lengo la kuifanya Tanzania kuwa na maendeleo endelevu, kuimarisha uchumi mkubwa (Macroeconomy) na kuwa na uchumi shirikishi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu